Monday, June 3, 2013

BRAZIL YALAZIMISHWA SARE YA 2-2 DHIDI YA ENGLAND KATIKA MECHI YA KIRAFIKI"

Katika Mechi ya ufunguzi rasmi Uwanja wa Maracana iliyopigwa jana  kati ya wenyeji brazil na England jina rasmi  la uwanja huo kwa sasa ni Estadio Jornalista Mário Filho huko Mjini Rio De Janeiro Wenyeji Brazil walilazimishwa  sare ya kufungana Bao 2-2 na England hapo jana Usiku.

Brazil walitawala Kipindi chote cha kwanza lakini hawakupata Bao hasa kutokana na kusimama imara kwa Kipa Joe Hart.

MAGOLI:

Brazil 2
-Fred Dakika ya 57
-Paulinho 82
-England 2
- Oxlade-Chamberlain Dakika ya 67
-Rooney 79
Bao zote 4 za Mechi hiyo ziliwekwa kimiani Kipindi cha Pili na Brazil ndio waliotangulia kufunga kupitia Fred lakini Alex Oxlade-Chamberlain alisawazisha Bao hilo.
mchezo huo ulikuwa ni wakati wa kukumbukwa sana  kutokana na Baba yake Mzazi Alex Oxlade-Chamberlain, Mark Chamberlain, aliekuwa Winga wa Stoke City, aliichezea England mara ya mwisho ilipocheza Maracana Mwaka 1984 na kuifunga Brazil Bao 2-0 katika Mechi ya Kirafiki.
England walikuwa kifua mbele kwa Bao 2-1 kwa Bao la Wayne Rooney kwa Shuti la Mita 25 huku zikiwa zimebaki Dakika 11 Mpira kwisha lakini Paulinho aliisawazishia Brazil Dakika 3 tu baadae.
MATOKEO MECHI NYINGINE ZA KIRAFIKI :
Lesotho 0 South Africa 2
Sudan 0 Tanzania 0
Algeria 2 Burkina Faso 0
Ireland 4 Georgia 0
Ukraine 0 Cameroon 0
United States 4 Germany 3