Monday, June 3, 2013

PEREZ AWA RAIS WA NADRID KWA MARA NYINGINE TENA:

Rais wa Real madrid FLORENTINO Perez amechaguliwa kwa kipindi kingine tena katika nafasi ya urais wa klabu hiyo katika mkutano wa uchaguzi uliofanyika mapema leo. mchakato wa uteuzi wa majina lilimalizika Jumamosi usiku wakati muda wa kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo ulipomalizika bila ya kutokea mgombea yoyote wa kushindana na Perez. Kutokana na hilo bodi ya uchaguzi ya klabu hiyo ilimpitisha na kumpigia kura kama mgombea pekee kwenye uchaguzi huo na baadae kutoa taarifa kupitia katika mtandao wake. Perez mweye umri wa miaka 66 ameiongoza klabu hiyo toka mwaka 2000.