Monday, June 3, 2013

CHELSEA YAMTAMBULISHA RASMI MTU SPESHO"MOURINHO"

KLABU ya soka ya Chelsea imemteua rasmi Jose Mourinho kuwa meneja wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka minne. Mourinho ambaye ni raia wa Ureno atachukua nafasi ya Rafael banitez aliyejiunga na Napoli baada ya kuinoa klabu hiyo kwa miezi sita. Hii ni mara ya pili kwa Mourinho kurejea Stamford Brigde kama kocha kocha baada ya kuondoka miaka sita iliyopita. Mourinho ndiye alikuwa chaguo la kwanza la mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich baada ya kuinunua klabu hiyo mwaka 2003 na ndiye kocha pekee kati ya tisa waliopita klabuni hapo kuanzia kipindi hicho aliyeipa mafanikio zaidi.
MAMENEJA WA CHELSEA CHINI YA ROMAN ABRAMOVICH:
-Claudio Ranieri: Sep 2000 mpaka Mei 2004
-Jose Mourinho: Jun 2004 mpaka Sep 2007
-Avram Grant: Sep 2007 mpaka Mei 2008
-Luiz Felipe Scolari: Jul 2008 mpaka Feb 2009
-Guus Hiddink: Feb 2009 mpaka Mei 2009
-Carlo Ancelotti: Jun 2009 mpaka Mei 2011
-Andre Villas-Boas: Jun 2011 mpaka Machi 2012
-Roberto Di Matteo: Machi 2012 mpaka Nov 2012
-Rafael Benitez: Nov 2012 mpaka Mei 2013
-Jose Mourinho: Juni 2013 -

Mourinho anarejea kwa mara nyingine Chelsea na kuwakuta tena baadhi ya Wachezaji aliokuwa nao mara ya kwanza kina Petr Cech, Ashley Cole, Frank Lampard, John Mikel Obi na John Terry pamoja na Michael Essien ambae alikuwa nae huko Real alikopelekwa kwa Mkopo na Chelsea.
Akizungumza kuhusu Mourinho, Mchezaji mkongwe wa Chelsea, Frank Lampard, alisema: “Ni Meneja Bora! Nimesema hili zaidi ya mara milioni, kiasi cha kuonekana kero kwa Watu, lakini nimebahatika kufanya nae kazi!”