Thursday, June 6, 2013

SPAIN BADO NAMBA MOJA UBORA DUNIANI - FIFA

Mabingwa wa Dunia timu ya taifa ya Spain bado ndio inaendelea kushika namba moja katika Listi ya viwango vya FIFA vya Ubora Duniani iliyotolewa leo ikifuatiwa na timu ya taifa ya ujerumani ambapo nafasi ya tatu inashikiliwa na  Argentina  ambapo nafasi ya nne ikishikiliwa na  Croatia, huku Tanzania Taifa star ikipanda Nafasi 7 kutoka 116 hadi 109.
Katika 10 Bora, Netherlands imepanda  mpaka Nafasi ya 5, Portugal kushuka Nafasi moja hadi ya 6, Colombia, wameshuka Nafasi 2 na wapo nafasi ya 7 huku timu ya taifa ya England ikiporomoka Nafasi 2 na sasa wako Nafasi ya 9.
Kwa Nchi za Afrika, Côte d'Ivoire ndio ipo Nafasi ya juu kabisa ikiwa Nafasi ya 13 ikifuatiwa na Ghana iliyokatika Nafasi ya 20.
Brazil, ambayo imeathirika kwa kucheza Mechi za Kirafiki tu kwa Miaka miwili, imeporomoka Nafasi 2  hadi Nafasi ya 22 lakini kushiriki kwao katika Mashindano rasmi ya FIFA ya kugombea Kombe la Mabara yatakayochezwa Nchini brazil  kuanzia Juni 15 kama watafanya vizuri basi itawaletea faida nzuri na sana katika harakati za kupanda chati.
Toleo jingine la Listi ya FIFA ya Ubora Duniani litatolewa Julai 4.
25 BORA:
1        Spain
2        Germany
3        Argentina
4        Croatia
5        Netherlands
6        Portugal
7        Colombia
8        Italy
9        England
10      Ecuador
11      Russia
12      Belgium
13      Côte d'Ivoire
14      Switzerland
15      Bosnia-Herzegovina
16      Greece
17      Mexico
18      France
19      Uruguay
20      Denmark
21      Ghana
22      Brazil
23      Mali
24      Czech Republic
25      Chile
NCHI ZINAZOIZUNGUKA TANZANIA:
104    Qatar
105    Lithuania
106    Ethiopia
107    Niger
108    Saudi Arabia
109    Malawi
109    Tanzania {imepanda nafasi 7]
111    Kuwait
112    Tajikistan
113    Suriname
114    Korea DPR
115    Benin 308
116    Northern Ireland