Thursday, June 6, 2013

GALLIANI ASEMA HATUNA MPANDO NA KAKA KUJA MILAN.

Adriano Galliani ambaye ni ofisa mkuu wa klabu ya AC Milan ya Italia,ametanabaisha na kuweka wazi kuwa klabu hiyo haina mpango wa kumsajili kiungo wa klabu ya Real Madrid Kaka ambapo amesema mchezaji huyo ameshakuwa mtu mzima. Kaka mwenye umri wa miaka 31 amekuwa akihusishwa na tetesi za kurejea San Siro kwa zaidi ya mara moja toka alipoondoka Milan kwenda Madrid mwaka 2009 lakini Galliani amekanusha tetesi hizo za kumsajili nyota huyo kutokana na umri wake. Kiungo huyo mshambuliaji bado ana mkataba na Madrid naomalizika katika kipindi majira ya kiangazi mwaka 2015 lakini anategemewa kuondoka katika klabu hiyo kutokana na kushindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza kwa miaka kadhaa sasa. Kaka amecheza mechi 19 pekee katika msimu wa 2012-2013 na kufunga mabao matatu.