Tuesday, June 11, 2013

MOYES AWEKA NIA YA DHATI KWA FABREGAS VS LEWANDOWSKI.

Mabingwa wa ligi kuu BPL nchini uingereza Msimu 2012-2013 hivi karibuni Club ya Manchester United imeongeza hali  na kasi ya kujiamini kuwa wanaweza kuwatwaa wachezaji Cesc Fabregas na Robert Lewandowski  kutua Old Trafford majira haya ya joto.
Kocha mpya wa United, David Moyes ametanabaisha kuwa angependa kuwasajili wote.
 kiungo wa Barcelona na mshambuliaji wa Kipoland wa Borussia Dortmund katika klabu yake kabla ya kikosi chake hakijakwenda katika ziara ya Asia na Australia katikati ya mwezi ujao.
Inafahamika kwamba, wachezaji wote hao wameonyesha nia zao za kuhamishia cheche zao kwa mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England, hivyo United wanaweza kufanikisha dili hizo.
Double strike: Man United believe they can land Cesc Fabregas and Robert Lewandowski (below)

Man United wanaamini wanaweza kumnasa Cesc Fabregas na Robert Lewandowski (chini)
Robert Lewandowski
Robert Lewandowski

Klabu yake ya zamani Fabregas, Arsenal haijaonyesha nia na malengo ya  kumsajili tena iwapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ataondoka Nou Camp, lakini United inafahamika wanamtaka kwa dhati kiungo huyo aliyeichezea kwa miaka nane timu hiyo ya London kabla ya kurejea Hispania miaka miwili iliyopita.
 
Lewandowski anaweza kuhamia England baada ya matumaini yake kuhamia kwa mabingwa wapya wa Ulaya, Bayern Munich kukatwa wiki hii.
United wamekuwa wakimfuatilia mshambuliaji huyo wa Poland kwa miezi kadhaa na wanaamini anaweza kuzalisha ushindani mzuri kwa Robin van Persie, ambaye atatimiza miaka 30 muda mfupi kabla timu haijaanza kutetea ubingw awake Agosti.

Changamoto: Robin van Persie anaweza kukabiliana na changamoto kubwa mwanzoni mwa msimu ujao Man United
Kuwasili kwake pia kunaweza kukuza shinikizo kwa Wayne Rooney ambaye ameomba kuondoka Old Trafford tangu mwishoni mwa msimu uliopita.