Tuesday, June 11, 2013

SNEIJDER ASIKITISHWA KUNYANG'ANYWA UNAHODHA:

KIUNGO nyota wa klabu ya Galatasaray  na timu ya taifa ya Uholanzi Wesley Sneijder amekiri kusikitishwa na kitendo cha kunyang’anywa kitambaa cha unahodha wa timu yake ya taifa. Kiungo huyo alipewa unahodha wa Uholanzi wakati Louis van Gaal alipochukua nafasi ya Bert van Marwijk baada ya michuano ya Ulaya 2012. Akihojiwa Sneijder amesema ni jambo lililomuumiza sana na sio sababu hakutambua hilo ila kwasababu amekua akijitoa kwa uwezo wake wote toka akabidhiwe majukumu hayo lakini inabidi akubaliane na uamuzi wa kocha. Baada ya kumvua unahodha kiungo huyo kutokana na kutofurahishwa na kiwango chake, Van Gaal alimkabidhi majukumu hayo mshambuliaji nyota wa Manchester United Robin van Persie ambaye ameisadia klabu yake kushinda taji la Ligi Kuu msimu uliopita.