Tuesday, June 11, 2013

ZINEDINE ZIDANE AWEKA WAZI KUWA WATAKA KUVUNJA REKODI YA USAJILI.

Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya REAL MADRID ambaye alikuwa kiungo wa wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Real Madrid, Zinedine Zidane amekiri kuwa lengo kuu ni kuvunja rekodi ya uhamisho kama watkuwa na nia ya kumsajili Gareth Bale. 
Bale ambaye ni winga wa klabu ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Madrid ambapo kuna taarifa kuwa klabu hiyo imetenga kitita cha paundi milioni 85 kwa ajili yake.
Kama uhamisho huo ukifanyika utakuwa umevunja rekodi aliyoweka Cristiano Ronaldo wakati aliposajiliwa kutoka Manchester United kwa ada ya paundi milioni 80 miaka minne iliyopita. 
Zidane amesema kwa kiwango cha mchezaji huyo alichokionyesha msimu uliopita sio ajabu vilabu vingi kumuwania ndio maana anadhani itakuwa gharama kubwa kupata saini yake. 
Nyota huyo wa zamani aliendelea kusema kuwa kama klabu yoyote yenye uwezo wa kifedha itahitaji saini ya mchezaji huyo lazima watoe dau kubwa na hata kufikia kuvunja rekodi ili Tottenham waweze kumuachia.