Friday, July 19, 2013

MBUYU TWITE "MAJERUHI KUIKOSA URA'

Beki mahiri mwenye nguvu na kasi Mbuyi Twite ataikosa mechi ya keshokutwa wakati Yanga itakapowavaa URA, timu inayomilikiwa na kampuni ya watoza kodi ya mapato ya Uganda.

URA itakuwa nchini kucheza mechi mbili za kirafiki, ikianza na Simba kesho kabla ya kuivaa Yanga, keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Twite amesema ataikosa mechi hiyo kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti ingawa amekuwa akifanya mazoezi taratibu.

Awali Yanga ilikuwa icheze mechi ya kirafiki dhidi ya 3 Pillars ya Nigeria, jana lakini ikagundulika timmu hiyo ilikuwa bagumashi kupita kiasi.

TFF ikapoga stop mchezo huo kwa kuwa Wanigeria hao walikuwa wameokotana lakini walitaka kucheza na mabingwa wa Tanzania.