Tuesday, July 2, 2013

SERENA WILLIAMS ATOLEWA NJE KATIKA TENESI MICHUANO YA WIMBLEDON

MWANADADA nyota dunia katika tenisi kutoka Marekani, Serena Williams ametolewa nje katika michuano ya Wimbledon baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Sabine Lisicki wa Ujerumani kwa 6-2 1-6 6-4. Williams ambaye mbali na kupewa nafasi kubwa ya kunyakuwa taji hilo pia alikuwa bingwa mtetezi wa michuano hiyo aliyonyakuwa mwaka jana. Kwa upande mwingine bingwa wa zamani wa michuano hiyo Petra Kvitova alifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo baada ya kumgaragaza Carla Suarez wa Hispania kwa 7-5 6-3. Mashindano ya Wimbledon mwaka huu yamekuwa sio mazuri kwa nyota wengi wanaoshika nafasi za juu katika orodha za ubora wa mchezo huo duniani baada ya Maria Sharapova anayeshika namba mbili kuenguliwa katika mzunguko wa pili huku Victoria Azarenka anayeshika namba tatu yeye akijitoa baada ya kupata majeraha.