Tuesday, March 18, 2014

YANGA, AZAM KUUMANA VPL TAIFA

Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea kesho (Machi 19 mwaka huu) kwa mechi kati ya Yanga na Azam itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.
Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zitaanza kuuzwa saa 2 asubuhi katika magari maalumu kwenye vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Ubungo Terminal, mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Samora/Ohio, OilCom Ubungo, Buguruni Shell, Dar Live- Mbagala, kituo cha daladala Mwenge na Uwanja wa Taifa.
Baada ya saa 6 mchana mauzo yote yatahamia Uwanja wa Taifa ambapo milango kwa ajili ya mechi itakuwa wazi kuanzia saa 7.30 mchana.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 30,000 kwa VIP A, sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani kiingilio ni sh. 7,000.
Mechi hiyo itachezeshwa na mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar es Salaam ambapo atasaidiwa na Anold Bugado (Singida), Florentina Zablon (Dodoma) na Lulu Mushi (Dar es Salaam). Kamishna wa mechi hiyo Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathimini wa waamuzi ni Alfred Rwiza wa Mwanza.
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
19
12
7
0
27
43
2
Yanga SC
18
11
6
1
29
39
3
Mbeya City
21
10
9
2
10
39
4
Simba SC
21
9
9
3
17
36
5
Kagera Sugar
21
8
8
5
3
32
6
Ruvu Shooting
20
7
7
6
-4
28
7
Coastal Union
21
5
11
5
1
26
8
Mtibwa Sugar
21
6
8
7
-1
26
9
JKT Ruvu
21
8
1
12
-13
25
10
Prisons FC
20
3
10
7
-4
19
11
Mgambo JKT
20
4
6
10
-17
18
12
Ashanti United
21
4
6
11
-18
18
13
JKT Oljoro
21
2
9
10
-16
15
14
Rhino Rangers
21
2
7
12
-14
13
RATIBA MECHI:
Jumatano Machi 19
Yanga v Azam FC
Jumamosi Machi 22
JKT Ruvu v Mbeya City
Rhino Rangers v Yanga
Kagera Sugar v Tanzania Prisons
Jumapili Machi 23
Simba v Coastal Union
Mgambo JKT v Mtibwa Sugar
Ruvu Shooting v Ashanti United
Azam FC v JKT Oljoro