Tuesday, March 18, 2014

DROGBA KUFUMUA NYASI STAMFORD BRIDGE.

Mshambuliaji Mahiri wa Galatasaray ya Uturuki, akiwa na wenzake amefanya mazoezi kwenye Uwanja wa Stamford Bridge unaotumiwa na Chelsea. 
Mara tu baada ya mazoezi, Drogba amesema yuko tayari kwa ajili ya mechi ya leo dhidi ya kikosi hicho cha Jose Mourinho katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
"Nimerudi tena hapa, kwangu ni sehemu bora na yenye kumbukumbu nyingi sana. Lakini kama ni mechi, niko tayari," alisema Drogba.
Katika mechi ya kwanza jijini Istambul, timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1. Hivyo jibu litatapikana leo.
UEFA CHAMPIONZ LIGI

Raundi ya Mtoano ya Timu 16

RATIBA

MARUDIANO

[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]

[Saa za Bongo]

Jumanne Machi 18

22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü [1-1]

22:45 Real Madrid CF v Schalke 04 [1-6]

Jumatano Machi 19

22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg [4-2]

22:45 Manchester United v Olympiacos CFP [0-2]