Tuesday, April 1, 2014

CAF KOMBE LA SHIRIKISHO: DROO RAUNDI YA MCHUJO YACHUKUWA NAFASI LEO

DROO ya Raundi ya Mchujo ya Mashindanoya CAF ya Kombe la Shirikisho imefanywa Leo huko Mjini Cairo, Misri na kuibua Mechi za mvuto ikiwemo Dabi ya Jiji la Bamako huko Nchini Mali.
Droo hii ilihusisha Timu 8 zilizoshinda Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Kombe la Shirikisho na Timu 8 zilizotolewa kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya CAF CHAMPIONZ LIGI.
Waliokuwa Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri, ambao walibwagwa na Al Ahly Benghazi ya Libya kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI na kutupwa Kombe la Shirikisho, wamepangiwa kucheza na Klabu ya Morocco, Difaa El Jadida.
Dabi ya Jiji lCAF-LOGO14a Bamako, itahusisha Klabu za huko Nchini Mali, Real Bamako, iliyotokea CAF CHAMPIONZ LIGI, dhidi ya Djoliba.
Mechi za Raundi ya Mchujo zitachezwa Aprili 18 na Marudiano Wiki moja baadae na Washindi 8 wataingizwa kwenye Droo ya Makundi ambapo Makundi mawili ya Timu 4 kila moja yatapangwa.
CAF Kombe la Shirikisho
Raundi ya Mchujo
Al Ahly (Egypt) vs Difaa El Jadida (Morocco)
Real Bamako (Mali) vs Djoliba (Mali)
AC Leopards (Congo) vs Medeama (Ghana)
Kaizer Chiefs (South Africa) vs ASEC Mimosas (Cote d'Ivoire)
Coton Sport (Cameroon) vs Petro Luanda (Angola)
Horoya (Guinea) vs ES Tunis (Tunisia)
Sewe Sport (Cote d'Ivoire) vs Bayelsa United (Nigeria)
Nkana (Zambia) vs Bizertin (Tunisia).
**Mechi kuchezwa Aprili 18 na Marudiano Wiki moja baadae
**Washindi 8 kuingizwa Droo ya Kupanga Makundi mawili