Tuesday, April 1, 2014

UCL:KAZI IPO MAN UNITED VS BAYERN MUNICH,BARCA KUIKABIRI ATLETICO MADRID

ROBO FAINALI
Robo Fainali
Mechi za Kwanza
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumanne Aprili 1
Barcelona v Atletico Madrid
Manchester United v Bayern Munich
Leo Usiku Uwanja wa Old Trafford huko Jijini Manchester utashuhudia mtanange mkali kati ya Mabingwa wa England, Manchester United, na Mabingwa wa Ulaya, ambao pia ndio Mabingwa wa Germany, Bayern Munich, katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL.
Mara ya mwisho kukutana kwa Timu hizi kwenye Michuano ya Ulaya ni Mwaka 2010 wakati Bayern Munich ilipoitoa Man United kwenye Robo Fainali kwa Bao za Ugenini.
Safari hii, hali ipo tofauti kwani Man United wanaingia kwenye Mechi hii huku Wachambuzi wengi hawawapi matumaini makubwa ya kufanya viziru dhidi ya Bayern Munich inayosifiwa kuwa ndio Timu Bora Ulaya hivi sasa na Juzi ilitwaa tena Ubingwa wa Germany huku wakiwa na Mechi 7 mkononi wakati Man United wanasuasua kwenye Ligi Kuu England wakiwa Nafasi ya 7.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
ROBO FAINALI
Robo Fainali
Jumatano Aprili 2
Real Madrid v Borussia Dortmund
Paris Saint-Germain v Chelsea
Marudiano
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumanne Aprili 8
Chelsea v Paris Saint-Germain
Borussia Dortmund v Real Madrid
Jumatano Aprili 9
Bayern Munich v Manchester United
Atletico Madrid v Barcelona
-DROO YA NUSU FAINALI: 11 Aprili
-Mechi kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
WASHINDI [Miaka ya karibu]:
MSIMU
MSHINDI
NCHI
MSHINDI WA PILI
NCHI
GOLI
2012-13
Bayern Munich
Germany
Borussia Dortmund
Germany
2-1
2011-12
Chelsea
England
Bayern Munich
Germany
1-1 (4–3)
2010-11
Barcelona
Spain
Manchester United
England
3-1
2009-10
Internazionale
Italy
Bayern Munich
Germany
2-0
2008-09
Barcelona
Spain
Manchester United
England
2-0
2007-08
Man United
England
Chelsea
England
1-1 (6–5)
UEFA CHAMPIONZ LIGI
WAFUNGAJI BORA 2013/14:
C. Ronaldo-Real Madrid Goli 13
Zlatan Ibrahimovic-PSG Goli 10 [Penati 1]
Messi-Barcelona Goli 8 [Penati 2]
Diego Costa-Atletico Madrid Goli 7
Sergio Agüero-Manchester City Goli 6 [Penati 2]