DROO za kupanga Makundi ya CAF CHAMPIONZ LIGI na Kombe la Shirikisho itafanyika Jumanne Aprili 29 huko Makao Makuu ya CAF Jijini Cairo Nchini Misri.
Kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI zipo Timu 8
zilizofuzu hatua hii na Droo hiyo itapanga Makundi mawili ya Timu 4 kila
moja ambayo yatacheza mtindo wa Ligi, Nyumbani na Ugenini, ili kupata
Timu mbili za juu toka kila Kundi kucheza Nusu Fainali.
Timu hizo 8 ni:
-Al-Ahly Benghazi ya Libya
-Al-Hilal ya Sudan
-AS Vita Club ya Congo DR
-CS Sfaxien ya Tunisia
-Espérance de Tunis ya Tunisia
-ES Sétif ya Algeria
-TP Mazembe ya Congo DR
-Zamalek ya Egypt
Mechi za Makundi zitaanza Wikiendi ya Mei 16 hadi 18.
CAF Kombe la Shirikisho
Kwenye CAF Kombe la Shirikisho, Droo ya
hapo kesho Jumanne pia itashirikisha Timu 8 ambazo nazo zitagawanywa
Makundi mawili ya Timu 4 kila moja ambayo yatacheza mtindo wa Ligi,
Nyumbani na Ugenini, ili kupata Timu mbili za juu toka kila Kundi
kucheza Nusu Fainali.
Timu hizo 8 ni:
-Sewe Sport - Ivory Coast
-Al Ahly – Egypt
-AS Real de Bamako – Mali
-AC Leopards de Dolisie – Congo
-ASEC Mimosas Abidjan - Ivory Coast
-Coton Sport FC – Cameroon
-E.S. Sahel – Tunisia
Mechi za Makundi zitaanza Wikiendi ya M
ei 16 hadi 18.
Marudiano
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumamosi Aprili 26
Bayelsa United – Nigeria 0 Sewe Sport - Ivory Coast 1 [0-3]
Difaa Hassani El Jadidi – Morocco 2 Al Ahly – Egypt 1 [2-2, Al Ahly yasonga kwa Bao la Ugenini]
Jumapili Aprili 26
Djoliba AC – Mali 0 AS Real de Bamako – Mali 0 [1-2]
Medeama – Ghana 2 AC Leopards de Dolisie – Congo 0 [2-2, Penati 4-5]
ASEC Mimosas Abidjan - Ivory Coast 1 Kaizer Chiefs - South Africa 0 [3-1]
Petro Atlético de Luanda - Angola 2 Coton Sport FC – Cameroon 2 [3-4]
E.S. Sahel – Tunisia 1 Horoya Athlétique Club – Guinea 0 [1-0]
C. A. Bizertin – Tunisia 1 Nkana FC – Zamba 1 [1-1]