Klabu ya Chelsea imekubali kutoa
kiasi cha pauni milioni 32 kwa Atletico Madrid kwaajili ya kukamilisha
dili la kumsajili mshambuliji mahiri,Diego Costa.
Costa ambaye amekuwa muhimili mkubwa kwa klabu
hiyo ya Uhispania ikiwa na uwezo wa kuchukua La Liga na Ligi ya
mabingwa barani Ulaya mpaka sasa, amekuwa akihusishwa na kuhamia London
huku Jose Mourinho akihitaji mshambuliaji hatari zaidi.

Dili la Costa halitarajiwi kutangazwa rasmi mpaka ifikapo mapema
mwezi Juni mara baada ya michezo miwili mikubwa ambayo nyota huyo
anapambana kuweza kuwa fiti kuisaidia timu yake.
Costa alipata majeraha ya misuli na alikosa mchezo waliotoka sare ya
1-1 dhidi ya Malaga Jumapili,mchezo ambao iwapo Atletico wangeshinda
wangekuwa
tayari wametwaa taji la La Liga msimu huu.
Atletico watasafiri mpaka Camp Nou kupambana na Barcelona siku ya
Jumapili katika mchezo ambao utaamua kombe linaenda wapi na siku saba
baadae watakutana na wapinzani wao wa Jiji,Real Madrid kwenye fainali ya
ligi ya mabingwa barani Ulaya itakayopigwa Lisbon.
Chelsea walimaliza msimu wa 2013/14 katika nafasi ya tatu,pointi nne
nyuma ya Manchester City na pointi mbili nyuma ya Liverpool huku rekodi
yao ya kufunga magoli ikionekana ndiyo sababu ya kushindwa kwao kupata
taji.

mhimili ambaye ni kiungo mshambuliaji Eden Hazard akifunga magoli 14.
Samuel Eto’o,Fernando Torres na Demba Ba walifunga jumla ya magoli 19
pekee wote kati yao hivyo kumshawishi Mourinho kutumia pesa nyingi
kwaajili ya kupata saini ya mchezaji kama Costa ambaye amefunga magoli
27 kwenye michezo 33 ya La Liga msimu huu.