Tuesday, May 13, 2014

HASSAN DALALI AWAPA SOMO WANACHAMA WA MSIMBA SC


Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Hassan Dalali, amewapa somo wanachama wa klabu hiyo kuwa makini katika kuelekea kwenye Uchaguzi huo.
Akizungumzia hilo jijini Dar es Salaam, Dalali alisema kuwa sio wote wanastahili ku
wa viongozi wa klabu hiyo kongwe ambayo kwa sasa imepoteza hadhi yake.
Alisema alipokuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, aliweza kuwaunganisha wana Simba, hivyo kunastahili kiongozi mwingine mwenye mfano wake.
“Hii Simba sasa imepoteza hadhi na heshima yake katika nyanja ya soka, hivyo lazima apatikane kiongozi imara na mwenye uwezo wa kuitumikia usiku na mchana.
“Tunahitaji kupata viongozi makini hivyo siku ya Uchaguzi na wakati huu lazima tuwapime wagombea wote kwasababu tunawajua vizuri,” alisema.
Kwa mujibu wa Dalali, baadhi ya wagombea hawana hadhi na uwezo wa kuwa rais wa kwanza wa klabu hiyo, kutokana na fikra zao kuwa fupi.