RAIS wa shirikisho la soka nchini Tanzania, Jamal Malinzi
imepigana kiume kuwasiliana na mwenyekiti na mmiliki wa klabu ya TP Mazembe,
Moise Katumbi na taarifa njema juu ya mawasiliano hayo ni kwamba
washambuliaji wawili wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas
Ulimwengu watawasili jumamosi mchana kwa ajili ya mchezo wa jumapili.

Nyota hao wawili
watatumiwa kwa mara ya kwanza na kocha wa Taifa stars, Mart Nooij katika mechi
ya raundi ya awali kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika mwakani nchini
Morocco dhidi ya Zimbabwe kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam