Thursday, June 5, 2014

CECAFA NILE BASIN CUP: VICTORIA UNIVERSITY BINGWA, WAULA DOLA 30,000!!


UNI2
UNI1VICTORIA UNIVERSITY wamefanikiwa kuwa Mabingwa wa Mashindano mapya ya CECAFA NILE BASIN CUP baada kuichapa AFC Leopards ya Kenya Bao 2-1 katika Fainali iliyochezwa huko Khartoum International Stadium Jijini Khartoum Nchini Sudan hapo Jana.
Haya ni Mashindano ya kwanza kabisa ya Kombe hilo yaliyoshindaniwa na Klabu kadhaa toka Nchi za Afrika Mashariki na ya Kati ambao ni Wanachama wa CECAFA.
Kwa ushindi huo, Victoria University pia wamejinyakulia Donge nono la Dola 30,000 na ni baraka kwa Klabu changa iliyoshiriki michuano ya CECAFA kwa mara ya kwanza kabisa.
Victoria University ndio waliowatoa Wawakilishi wa Tanzania Bara, Mbeya City, kwenye Robo Fainali baada ya kuwafunga Bao 1-0 kwa Bao la Penati.
UNI3Kwa kuwa Washindi wa Pili, AFC Leopards walipewa Dola 20,000.
MAGOLI:
Victoria University 2
-Odongo Mathew Dakika ya 29
-Mutyaba Muzamir 90+2
AFC Leopards 1
-Ikene Austin Dakika ya 45

Nao, Timu ya Sudan, Al Shandy, ilinyakua Dola 10,000 kwa kumaliza Washindi wa Tatu baada ya kuifunga Academie Tchite ya Burundi Bao 4-1.
Klabu zilizoshiriki muchuano hii ni:
KUNDI A
-Polisi [Zanzibar]
-Victoria University Uganda]
-Malakia [South Sudan]
Al Merreikh [Sdan]
KUNDI B
-Mbeya City [Tanzania Bara]
-AFC Leopards [Kenya]
-Academie Tchite [Burundi]
-Enticelles [Rwanda]
KUNDI C
-Defence [Ethiopia]
-Dkhill FC [Djibouti]
-Al Shandy [Sudan]