Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea taarifa za kutolewa wito bungeni wa kulitaka litumie tiketi za elektroniki katika kukusanya mapato.

Katika mpira wa miguu wanaingia maelfu
ya watu katika kipindi kifupi. Kwa kuzingatia umuhimu wa kulinda usalama
wa watazamaji na miundombinu ya viwanja ndio maana tulisitisha matumizi
ya tiketi za elektroniki hadi tujihakikishie usalama wa matumizi yake.
Tunafanya jitihada kwa karibu na mzabuni benki ya CRDB ili kuhakikisha mfumo huu unaanza kutumika mara moja.
Kwa niaba ya sekta ya michezo tunatoa
wito kwa Serikali kushusha au kuondoa kodi kubwa zinazotozwa kwenye
vifaa vya michezo, hasa vinavyotumiwa na watoto kuanzia umri wa miaka
6-12, ili watoto wetu waweze kuvipata kirahisi toka kwa wazazi wao ili
waweze kujifunza kucheza michezo kisasa tangu wakiwa wadogo.
TAIFA STARS KUINGIA KAMBINI JUNI 11
Kikosi cha Taifa Stars kinaingia tena
kambini Jumatano (Juni 11 mwaka huu) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya
mechi ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika dhidi ya Msumbiji
itakayochezwa Julai 20 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro
Premium Lager itakuwa na kambi ya siku tatu jijini Dar es Salaam
ikijumuisha wachezaji 28. Kwa mujibu wa programu ya Kocha Mart Nooij,
Stars itaingia tena kambini Juni 24 mwaka huu.
Wachezaji wanaotakiwa kuripoti kambini
ni Deogratias Munishi, Aishi Manula, Benedictor Tinoko, Kelvin Yondani,
Said Moradi, Nadir Haroub, Joram Nason, Shomari Kapombe, Oscar Joshua,
Edward Charles, Aggrey Morris na Pato Ngonyani.
Wengine ni Mwinyi Kazimoto, Frank
Domayo, Amri Kiemba, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Said Juma, Haruna
Chanongo, Himid Mao, Said Ndemla, John Bocco, Simon Msuva, Kelvin
Friday, Ramadhan Singano, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa na Mwegane Yeya.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)