Friday, June 27, 2014

SIMBA SC YAWAALIKA WADAU KUONA MAENDELEO YA UWANJA BUNJU



SIMBA wekundu wa msimbazi wamesema kuwa sasa wapo katika kuondoa dhama kama club kongwe ilianzishwa mwaka 1936 kuhakikisha wanakamilisha uwanja huo.
hivyo basi wameamua kuwaalika wanachama wanahabari kuona maendeleo ya uwanja wa Bunju Jinsi unavyo endelea ambapo sasa umefika hatua nzuri kilicho baki ni kuanza kuweka nyasi.

Yote  kwa yote Azam fc kwa hapa tz ndio timu pekee ndio klabu ya Tanzania yenye uwanja wake wa kisasa kwa ajili ya mazoezi, mechi za ligi kuu na michuano yote inayosimamiwa na shirikisho la soka barani Afrika, CAF.
Katika historia ya soka la Tanzania, Azam fc haiwezi kunusa ukongwe wa klabu mbili za Simba na Yanga.
Hizi ni klabu zenye mafanikio ndani na nje ya uwanja. Ni klabu zenye mashabiki kila kona ya nchi hii.
Lakini licha ya kukaa miaka mingi katika soka la ushindani nchini Tanzania na michuano ya Kimataifa, Yanga na Simba hazijawahi kumiliki viwanja vyake vya mazoezi na mechi za ligi kuu.
Kwa miaka mingi sasa viongozi wanaopita katika klabu hizo wanakuja na ndoto za kujenga viwanja, lakini zinayeyuka kutokana sababu mbalimbali ikiwemo kuendekeza siasa kuliko vitendo.