Tuesday, July 22, 2014

CECAFA KAGAME CUP: RATIBA HADHARANIYANGA KUANZA NA RAYON!

Ratiba ya Mashindano ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA KAGAME CUP, ambayo yatachua nafasi huko Kigali Nchini Rwanda kuanzia Agosti 8 na kumalizika Agosti 24.
Yanga, ambao walipangwa Kundi A, wataanza kwa kuivaa Rayon Sports ya Rwanda kwenye Uwanja wa Amahoro, Kigali hapo Ijumaa Agosti 8.
KMKM ya Zanzibar, ambao wako Kundi moja na Yanga, wataanza kwa kuivaa Atlabara ya South Sudan Siku hiyohiyo Agosti 8 kwenye Uwanja wa Nyamirambo huko Kigali.
MAKUNDI:
KUNDI A
-Rayon Sports [Rwanda]
-Yanga [Tanzania]
-Coffee [Ethiopia]
­-Atlabara [South Sudan]
-KMKM [Zanzibar]
KUNDI B
-APR FC [Rwanda]
-KCCA [Uganda]
-Flambeau de l'est [Burundi]
-Gor Mahia [Kenya]
-Telecom [Djibouti]
KUNDI C
-Vital'O [Burundi]
-El Merreikh [Sudan]
-Benadir [Somalia]
-Polisi [Rwanda]
Michezo yote zitachezwa Mjini Kigali kwenye Viwanja vya Amahoro na Nyamirambo huku Rubavu ikiwa ni Uwanja wa Akiba.
Tangu Mwaka 2002 Mdhamini wake mkuu ni Rais Paul Kagame wa Rwanda ambae amekuwa akitoa Dola 60,000 kila Mwaka.
Mashindano haya yatarushwa moja kwa moja kwenye TV na SuperSport International ambacho hivi karibuni kilisaini Mkataba wa Miaka Minne na CECAFA.
Ratiba kamili itatolewa baadae na CECAFA baada Timu zote kuthibitisha kushiriki.
Mbali ya kutwaa Kombe, Bingwa wa Kagame Cup huzoa Donge la Dola 30,000, Mshindi wa Pili Dola 20,000 na Timu ya Tatu hupata Dola 10,000.
RATIBA KAMILI:
TAREHE NA MECHI KUNDI UWANJA
Ijumaa Agosti 8 1 Atlabara v KMKM A NYAMIRAMBO
2 Rayon v Yanga A AMAHORO
3 Gor Mahia v KCCA B AMAHORO
Jumamosi Agosti 9 4 Vital ‘O’ v Banadir C AMAHORO
5 Police v El Mereikh C AMAHORO
6 APR v Flambeau B AMAHORO
Jumapili Agosti 10 7 KMKM v Young A AMAHORO
8 Telecom Vs KCCA B NYAMIRAMBO
9 Coffee v Rayon A AMAHORO
Jumatatu Agosti 11 10 Banadir v El Mareikh C NYAMIRAMBO
11 Gor Mahia v Flambeau B ‘’
12 Vital ’O’ v Police C ‘’
Jumanne Agosti 12 13 KMKM v Coffee A ‘’
14 Yanga v Atlabara A ‘’
Jumatano Agosti 13 15 APR  v Telecom B ‘’
16 KCCA v Flambeau B ‘’
Alhamisi Agosti 14 17 Coffee v Atlabara A
18 Rayon  v KMKM A
19 Police v Banadir C
Ijumaa Agosti 15 20 Flambeau v Telecom B
21 APR v Gor mahia B
22 El Mareikh v Vital ‘O’ C
Jumamosi Agosti 16 23 Coffee v Yanga A
24 Rayon v Atlabara A
Jumapili Agosti 17 25 Telecom v Gormahia B
26 KCC v APR B
Jumatatu Agosti 18 MAPUMZIKO

Jumanne Agosti 19 ROBO FAINALI

27 C1 v B3
NYAMIRAMBO
28 A1 v B2
‘’
Jumatano Agosti 20 29 A2 v C2
‘’
30 B1 v A3
‘’
Alhamisi Agosti 21 MAPUMZIKO

Ijumaa Agosti 22 NUSU FAINALI

31
32
Mshindi 27 v Mshindi 28
Mshindi 29 v Mshindi 30

AMAHORO
Jumamosi Agosti 23 MAPUMZIKO

Jumapili Agosti 24 MSHINDI WA 3 & FAINALI

33
34
Mfungwa 31 v Mfungwa 32
Mshindi 31 v Mshindi 32

AMAHORO
MUDA WA KUANZA MECHI UTAAMULIWA KATI YA CECAFA, FERWAFA NA SUPERSPORT KWA AJILI YA MATANGAZO LAIVU YA TV.

Sunday, July 20, 2014

STARS YALAZIMISHWA SARE 2-2 NA MAMBAS MSUMBIJI TAIFA

Timu ya taifa ya Tanzzania Taifa Stars Leo ikiwa katika dimba la uwanja wa taifa imejiweka katika wakatik mgumu kutinga Hatua ya Makundi ya kutafuta nafasi za kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, huko Morocco Mwakani, baada kutoka Sare 2-2 na Msumbiji kwenye Mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Stars, wakiwa chini ya Kocha Mart Nooij ambae kati ya Mwaka 2007 na 2011 alikuwa Kocha wa Msumbiji, walitanguliwa kufungwa kwa Bao la Penati iliyopigwa na Domingues lakini walijitutumua na kusawazisha kwa Bao la Mcha Khamis ambae pia alifunga Bao la Pili kwa Penati.
Hata hivyo, kazi hiyo njema ilipotea bure baada ya kuwaruhusu Msumbiji kusawazisha katika Dakika ya 89 kwa Bao la Isaac Carvalho.
MAGOLI:
Tanzania 2
-Mcha Khamis Dakika ya 66 & 71 [Penati]
Mozambique 2
-Gaspar Domingues Dakika ya 48 [Penati]
-Isac Carvalho 89

Kwenye Mechi nyingine iliyochezwa Leo huko Setsoto Stadium, Maseru, Wenyeji Lesotho waliifunga Kenya Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 70 la Moletsane.
Mechi za Marudiano zitachezwa Wikiendi ya Agosti 1 hadi 3.
AFCON 2015-MOROCCO
RATIBA/MATOKEO:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Julai 19
Uganda 2 Equatorial Guinea 0
Botswana 2 Guinea-Bissau 0
Sierra Leone 2 Seychelles 0
TFF-TANZANIA-MSUMBIJIJumapili Julai 20
Lesotho 1 Kenya 0
Tanzania 2 Mozambique 2
17:30 Congo v Rwanda
18:00 Benin v Malawi
** Mechi za Marudiano zitachezwa Wikiendi ya Agosti 1 hadi 3.
MAKUNDI:
KUNDI A
-Nigeria
-South Africa
-Sudan
-Mshindi Congo/Rwanda
KUNDI B
-Mali
-Algeria
-Ethiopia
Mshindi Benin/Malawi
KUNDI C
-Burkina Faso
-Angola
-Gabon
-Mshindi Lesotho/Kenya
KUNDI D
-Ivory Coast
-Cameroun
-Congo DR
-Mshindi Sierra Leone/Seychelles
KUNDI E
-Ghana
-Togo
-Guinea
Mshindi Uganda/Mauritania
KUNDI F
-Zambia
-Cape Verde
-Niger
-Mshindi Tanzania/Msumbiji
KUNDI G
-Tunisia
-Egypt
-Senegal
-Mshindi Botswana/Guinea-Bissau

MUJICA ASEMA SUAREZ ANAHITAJI DAKTARI SAIKILOGIASI KIFUNGO

RAIS wa Uruguay, Jose Mujica, bado ameendelea ameponda Kifungo cha Mchezaji wa Nchi hiyo Luis Suarez cha Miezi Minne alichopewa na FIFA na badala yake anahitaji msaada wa Madaktari wa Magonjwa ya Akili.
Suarez alifungiwa Miezi Minne kutojishughulisha na chochote kuhusu Soka na pia kufungiwa Mechi 9 za Uruguay baada kupatikana na hatia ya kumuuma Meno Beki wa Italy, Giorgio Chiellini, wakati wa Mechi ya Kombe la Dunia kati ya Uruguay na Italy huko Brazil hapo Juni 24.
Akiongea na Gazeti la Brazil, Folha de Sao Paulo, Rais Mujica, ambae ndie anasifika ya kuwa Rais ‘maskini’ kupita yeyote Duniani kwa uamuzi wake wa kuishi kwenye Banda la Shambani kwake badala ya Ikulu akilindwa na Polisi Wawili tu na Mbwa wake Manuela mwenye Miguu Mitatu, amesema: “Anatoka Familia fukara na akili yake ni Miguu yake. Ni bora kumpeleka Hospitali ambako atapata msaada
wa Daktari wa Magonjwa ya Akili!”
Rais Mujica amefafanua: “Ni wehu kumfungia Mtu asishiriki lolote kuhusu Soka! Hata Serikali haina mamlaka ya kumzuia Mtu asiingie Uwanja wa Mpira bila kupata Saini ya Jaji! Lakini FIFA wanakuja wanamfungia Miezi Minne bila hata kuwa na Jopo la Kisheria!”
Hivi sasa Suarez ameihama Klabu yake Liverpool ya England na kutua Barcelona ya Spain.
Na Rais Mujica amenung’unika: “Sasa tutamuona Suarez akicheza pamoja na Neymar na Messi lakini sijui lini itakuwa hivyo!”

SALAH UPO UWEZEKANO WA KUWEPO CHELSEA MATATANI AITWA KWAO MISRI

Mohamed Salah Mchezaji wa Chelsea huenda asiichezee tena Chelsea kwa Kipindi cha Miaka Mitatu baada ya kuitwa Nchini kwao ili aende Jeshini kwa Mujibu wa Sheria.
Taarifa kutoka Misri zimedai kuwa Salah, mwenye Miaka 22 na ambae alijiunga na Chelsea Mwezi Januari Mwaka huu kutoka Basle ya Uswisi, ameruhisiwa kuishi Nchini Uingereza kwa sababu anajihusisha na Masomo.
Hivi sasa imeripotiwa kuwa Wizara ya Elimu ya Juu ya Misri imefuta Masomo hayo na kumtaka arudi Misri mara moja ili atumikie Jeshini kwa Mujibu wa Sheria kwa Kipindi cha kuanzia Mwaka Mmoja hadi Mitatu.
Hata hivyo, Mchambuzi wa Soka kutoka Misri alisema vitu hivyo ni kawaida huko kwao na mara nyingi Mastaa wanaowakilisha vyema Nchi zao huruhusiwa kuendelea na shughuli zao bila bughudha.
Hivi sasa, Chama cha Soka cha Misri, Makocha wa Timu ya Taifa ya Misri na Maafisa wa Wizara ya Elimu ya Juu ya Misri, wameandaa Kikao ili kuangalia nini cha kufanya kuhusu Salah.
Vile vile, Meneja wa Timu ya Taifa ya Misri, Shawky Gharib, amemwomba Waziri wa Vijana kusaka suluhisho la tatizo hilo ili kumruhusuSalah arejee Misri Mwezi Septemba kuichezea Nchi hiyo kwenye Mechi za Makundi za kuwania Nafasi za kucheza Fainali za AFCON 2015 huko Morocco Mwakani.
Ikiwa hali ya sasa itaendelea Salah akirudi kwao tu hataruhusiwa kutoka nje ya Nchi hadi atumikie Jeshi kwa Kipindi hicho cha Mwaka mmoja hadi mitatu.


Mohamed Salah
Personal information
Full name Mohamed Salah Ghaly
Date of birth 15 June 1992 (age 22)
Place of birth Basion, El Gharbia, Egypt
Height 1.75 m (5 ft 9 in)
Playing position Winger
Timu ya sasa
Current team
Chelsea
Number 15
Timu za vijana
2006–2010 El Mokawloon
Timu za ukubwani
Years Team Mechi (Goli)
2010–2012 El Mokawloon 41 (11)
2012–2014 Basel 47 (9)
2014– Chelsea 10 (2)
Timu ya taifa
2010–2011 Egypt U20 11 (3)
2011–2012 Egypt U23 11 (4)
2011– Egypt 29 (17)