Sunday, July 20, 2014

SALAH UPO UWEZEKANO WA KUWEPO CHELSEA MATATANI AITWA KWAO MISRI

Mohamed Salah Mchezaji wa Chelsea huenda asiichezee tena Chelsea kwa Kipindi cha Miaka Mitatu baada ya kuitwa Nchini kwao ili aende Jeshini kwa Mujibu wa Sheria.
Taarifa kutoka Misri zimedai kuwa Salah, mwenye Miaka 22 na ambae alijiunga na Chelsea Mwezi Januari Mwaka huu kutoka Basle ya Uswisi, ameruhisiwa kuishi Nchini Uingereza kwa sababu anajihusisha na Masomo.
Hivi sasa imeripotiwa kuwa Wizara ya Elimu ya Juu ya Misri imefuta Masomo hayo na kumtaka arudi Misri mara moja ili atumikie Jeshini kwa Mujibu wa Sheria kwa Kipindi cha kuanzia Mwaka Mmoja hadi Mitatu.
Hata hivyo, Mchambuzi wa Soka kutoka Misri alisema vitu hivyo ni kawaida huko kwao na mara nyingi Mastaa wanaowakilisha vyema Nchi zao huruhusiwa kuendelea na shughuli zao bila bughudha.
Hivi sasa, Chama cha Soka cha Misri, Makocha wa Timu ya Taifa ya Misri na Maafisa wa Wizara ya Elimu ya Juu ya Misri, wameandaa Kikao ili kuangalia nini cha kufanya kuhusu Salah.
Vile vile, Meneja wa Timu ya Taifa ya Misri, Shawky Gharib, amemwomba Waziri wa Vijana kusaka suluhisho la tatizo hilo ili kumruhusuSalah arejee Misri Mwezi Septemba kuichezea Nchi hiyo kwenye Mechi za Makundi za kuwania Nafasi za kucheza Fainali za AFCON 2015 huko Morocco Mwakani.
Ikiwa hali ya sasa itaendelea Salah akirudi kwao tu hataruhusiwa kutoka nje ya Nchi hadi atumikie Jeshi kwa Kipindi hicho cha Mwaka mmoja hadi mitatu.


Mohamed Salah
Personal information
Full name Mohamed Salah Ghaly
Date of birth 15 June 1992 (age 22)
Place of birth Basion, El Gharbia, Egypt
Height 1.75 m (5 ft 9 in)
Playing position Winger
Timu ya sasa
Current team
Chelsea
Number 15
Timu za vijana
2006–2010 El Mokawloon
Timu za ukubwani
Years Team Mechi (Goli)
2010–2012 El Mokawloon 41 (11)
2012–2014 Basel 47 (9)
2014– Chelsea 10 (2)
Timu ya taifa
2010–2011 Egypt U20 11 (3)
2011–2012 Egypt U23 11 (4)
2011– Egypt 29 (17)