Timu ya taifa ya Tanzzania Taifa Stars Leo ikiwa katika dimba la uwanja wa taifa imejiweka katika wakatik mgumu
kutinga Hatua ya Makundi ya kutafuta nafasi za kucheza Fainali za
Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, huko Morocco Mwakani, baada kutoka Sare 2-2 na Msumbiji kwenye Mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Stars, wakiwa chini ya Kocha Mart Nooij ambae kati ya Mwaka 2007 na
2011 alikuwa Kocha wa Msumbiji, walitanguliwa kufungwa kwa Bao la Penati
iliyopigwa na Domingues lakini walijitutumua na kusawazisha kwa Bao la
Mcha Khamis ambae pia alifunga Bao la Pili kwa Penati.
Hata hivyo, kazi hiyo njema ilipotea bure baada ya kuwaruhusu
Msumbiji kusawazisha katika Dakika ya 89 kwa Bao la Isaac Carvalho.
Tanzania 2
-Mcha Khamis Dakika ya 66 & 71 [Penati]
Mozambique 2
-Gaspar Domingues Dakika ya 48 [Penati]
Kwenye Mechi nyingine iliyochezwa Leo huko Setsoto Stadium, Maseru,
Wenyeji Lesotho waliifunga Kenya Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 70 la
Moletsane.
Mechi za Marudiano zitachezwa Wikiendi ya Agosti 1 hadi 3.
AFCON 2015-MOROCCO
RATIBA/MATOKEO:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Julai 19
Uganda 2 Equatorial Guinea 0
Botswana 2 Guinea-Bissau 0
Sierra Leone 2 Seychelles 0
Lesotho 1 Kenya 0
Tanzania 2 Mozambique 2
17:30 Congo v Rwanda
18:00 Benin v Malawi
** Mechi za Marudiano zitachezwa Wikiendi ya Agosti 1 hadi 3.
MAKUNDI:
KUNDI A
-Nigeria
-South Africa
-Sudan
-Mshindi Congo/Rwanda
KUNDI B
-Mali
-Algeria
-Ethiopia
Mshindi Benin/Malawi
KUNDI C
-Burkina Faso
-Angola
-Gabon
-Mshindi Lesotho/Kenya
KUNDI D
-Ivory Coast
-Cameroun
-Congo DR
-Mshindi Sierra Leone/Seychelles
KUNDI E
-Ghana
-Togo
-Guinea
Mshindi Uganda/Mauritania
KUNDI F
-Zambia
-Cape Verde
-Niger
-Mshindi Tanzania/Msumbiji
KUNDI G
-Tunisia
-Egypt
-Senegal
-Mshindi Botswana/Guinea-Bissau