Tuesday, August 26, 2014

KOCHA WA POLISI MORO AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUJITUMA VPL.


Kocha Mkuu wa Polisi Morogoro Adolf’ Rishard ameweka wazi kuhusu timu yake timu yake ifanye vizuri msimu huu, wachezaji wanatakiwa wajitume, washikamane na kucheza kama timu moja.

Adolf ameyasema hayo wakati akizungumza na mtandao huu ambapo amesema ushindi unawezekana kama wachezaji wake watakuwa wanazingatia maelekezo wanayopewa.
Adolf amesema malengo yetu makubwa msimu ujao ni kufanya vizuri, na hayo yote yatawezekana kutokana na jinsi wachezaji watakavyojituma na kucheza kiushindani.
Katika kuhakikisha lengo linatimia tayari imeshafanya usajili wa wachezaji kadhaa wakiwamo Salum Machaku, Edward Chistopher aliyekuwa Simba, Dan Mrwanda, Labana Kambone wa Rhino Rangers, Toni Kavishe wa Mgambo JKT, Seleman Selembi wa Coastal Union na Mohamed Mpopo wa Villa Squad.