Adolf ameyasema hayo wakati akizungumza na mtandao huu ambapo amesema ushindi unawezekana kama wachezaji wake watakuwa wanazingatia maelekezo wanayopewa.
Katika kuhakikisha lengo linatimia tayari imeshafanya usajili wa wachezaji kadhaa wakiwamo Salum Machaku, Edward Chistopher aliyekuwa Simba, Dan Mrwanda, Labana Kambone wa Rhino Rangers, Toni Kavishe wa Mgambo JKT, Seleman Selembi wa Coastal Union na Mohamed Mpopo wa Villa Squad.