Kocha mkuu
Mbrazil kwenye Ligi ya Tanzania, Marcio Maximo ametamka kuwa anawajua wachezaji
watano tu wa kigeni Yanga na ndio atakaowatumia Miongoni mwao jina la Okwi
ambaye yupo Dar es Salaam halimo.

Pamoja
na wachezaji hao watano wanaofanya mazoezi ya pamoja, Yanga ina mkataba na Okwi
anayefanya timu kuwa na wachezaji sita wa kigeni idadi ambayo hadi kesho
Jumatano siku ya kufunga dirisha la usajili lazima ipunguzwe kwa mmoja kutupiwa
virago.

Okwi
ambaye alikuwa anapewa kipaumbele lakini alichelewa kujiunga na timu kwa sababu
zisizojulikana, inadaiwa kuwa uongozi umemwambia ajieleze kwa barua na baada ya
hapo atapewa adhabu ambayo ni siri.Okwi alichelewa kuja kambini kujiunga na Yanga kwa madai kwamba
hajalipwa fedha zake.
Kocha
Msaidizi wa Yanga, Leonardo Neiva ambaye pia ni Mbrazili amesema wamefurahishwa
na uwezo wa Kiiza na kukiri kuwa ana
sababu zote za kubaki Yanga.