Tuesday, August 26, 2014

NOOIJ AITA 26 STARS KUIKABILI MOROCCO SEPTEMBA 5 MWAKA HUU.

Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij ametangaza kikosi cha wachezaji 26 kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya FIFA Date dhidi
ya Morocco itakayochezwa Septemba 5 mwaka huu nchini Morocco.
Wachezaji walioitwa ni makipa Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Said Morad (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Shomari Kapombe (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Azam), Aggrey Morris (Azam), Joram Mgeveke (Simba) na Charles Edward (Yanga).
Viungo ni Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Liuzio 9ZESCO, Zambia).
Timu hiyo itaingia kambini Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) mchana katika hoteli ya Accomondia.
                      Mart Nooij
Taarifa Binafsi
Full nameMartinus Ignatius Nooij 
Date of birthJune 3, 1954 (age 60)
Place of birthHeemskerkNetherlands
Timu anayofundisha
Current team
Tanzania
Timu alizofundisha
YearsTeam
2003Burkina Faso U20
2007–2011Mozambique
2012Santos Cape Town
2013–2014Saint George
2014–Tanzania