
Bao pekee katika mchezo huo limefungwa na Mbrazil, Geilson Santos Santana ‘Jaja’ katika dakika ya 6 ya mchezo.
Hii ilikuwa mechi ya kwanza kwa kocha wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo kuwaona wachezaji wake wakicheza mechi ya kirafiki.
Ili kuhakikisha anawaona wachezaji wote, Maximo alitumia vikosi viwili tofauti kwa kila kipindi.