Monday, August 25, 2014

STARS KUKIPIGA NA MOROCCO DECEMBER 5 MWAKA HUU KIRAFIKI

Timu ya Tanzania Taifa Stars inataraji kwenda Morocco kukipiga na wenyeji wake katika mechi ya kirafiki ndani ya tarehe za Fifa.
Mechi hiyo imepangwa kuchezwa Septemba 5 nchini Morocco.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mwesigwa Celestine amesema wamepokea mwaliko na tayari Kocha Mart Nooij ameishatangaza kikosi chake.
Mwesingwa amesema Septemba 5 ni tarehe ambayo iko ndani ya tarehe za Fifa, hivyo maandalizi yanaanza na kocha ameishaita kikosi.

Stars katika mechi yake ya mwisho, Stars ilichapwa kwa mabao 2-1 ikiwa ugenini nchini Msumbuji na kutolewa katika mbio za kuwania kucheza michuano ya Mataifa Afrika.