Monday, August 25, 2014

TFF YAOMBA KUANDA MECHI ZA MASHINDANO YA AFCON 2017

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) chini ya Rais wake, Jamal Malinzi, limeomba kuadaa mashindano ya Kombe la Taifa Africa (Afcon).
TFF imetuma barua kwa Shirkisho la Soka Afrika (Caf) kuomba kuandaa mashindano yatakayofanyika 2017.

TFF imechukau uamuzi huo baada ya Caf kuifuta Libya iliyopanga kuandaa michuano hiyo mwaka 2017 kutokana na vurugu.

TFF imesema inaamini kuna miundombinu ya kutosha kuandaa michuano hiyo na tayari barua imetumwa Caf.
Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Celestine amesema barua ya maombi kwenda imeshatumwa.