Simba Wekundu wa msimbazi SC kesho wanatarajia kushuka dimbani kuonyeshana kazi katika Mechi ya pili ya kimataifa ya kirafiki chini ya kocha Patrick Phiri
dhidi ya timu ya mamlaka ya ukusanyaji wa mapato nchini Uganda, URA katika uwanja wa Taifa jijini Dar es slaam katika mtanange utakao anza majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za Afrika mashariki.
Wakati huo huo jumamosi jioni,
Simba itakuwa na mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Ndanda fc katika
uwanja wa Nangwanda Sijaona mk
oani Mtwara katika maadhimisho ya ‘Ndanda
fc Day’.