Thursday, September 11, 2014

MWAMBUSI ASEMA PHIRI, MAXIMO, ASEMA NGOMA DAKIKA 90.

KOCHA mkuu wa Mbeya City fc na kocha bora wa ligi kuu Tanzania bara msimu uliopita, Juma Mwambusi, amewakaribisha makocha Patrick Phiri wa Simba na Marcio Maximo wa Yanga.
Akizungumza na mtandao huu, Mwambusi amesema kocha Phiri ana historia ya kufundisha soka la Tanzania kwa ngazi ya klabu wakati Maximo amefundisha timu ya Taifa, lakini wote wataleta changamoto nzuri kwake.