Wednesday, September 10, 2014

JE TUFIKA KUHUSU TAIFA STARS HII AMA NDIO MWISHO

Hakuna kitu kinawaumiza watanzania kuhusu kilio kikubwa cha wadau na wapenzi wa soka nchini Tanzania ni kuitaka serikali, TFF na vyama wanachama wake pamoja na klabu zote kuwekeza katika soka la vijana kwa manufaa ya Taifa.
Tatizo la soka la Tanzania ni la kimfumo. Hakujawa na njia sahihi ya kupata wachezaji na kusababisha kuborongo kwa muda mrefu.
Aina ya wachezaji wanaopatikana Tanzania ni wale wasiokuwa na misingi ya mpira tangu utotoni, kwasababu hakuna akademi za kisasa na hata za kawaida kwa maeneo mengi ya nchi hii, hivyo vijana wenye vipaji vya soka hujikuta hawana kwa kujiendeleza.
Soka la vijana ni muhimu na lazima Taifa kama Taifa liandae mpango mkakati wa kitaifa kwa malengo ya kuwa na falsafa ya Taifa na mfumo sahihi wa kuibua, kukuza na kulinda vipaji vya soka.
Marsh aliachishwa kazi ya kuinoa Stars sambamba na kocha Mdenish, Kim Poulsen kwa madai ya wawili hao kushindwa kufikia malengo yaliyowekwa na Shirikisho la soka la Tanzania, TFF.
Hata hivyo wakati Kim anavunjiwa mkataba, Mashi alikuwa wodini akipata matibabu kutokana na kusumbuliwa na maradhi.
Usidhani huwa anakaa bure. Marsh ni moja ya watu wachache nchini wenye kiu ya kuona soka la nchi hii linapiga hatua.
Tangu mwaka 1991 anamiliki kituo chake cha kuibua, kulea na kukuza vipaji mkoani mwanza.