Wednesday, September 10, 2014

MAJIMAJI YAWEKA HADHARANI KIKOSI CHAKE KWA AJILI YA LIGI DARAJA LA KWANZA

 ya zamani Tanzania, Majimaji FC WANALIZOMBE ya Songea mkoani Ruvuma imetaja kikosi cha wachezaji 26 iliyowasajili kwa ajili ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara msimu wa 2014-2015.
Ofisa Habari wa Majimaji ya Songea, Nathan Mtega ametaja kikosi cha msimu ujaoAmesema katika kikosi hicho, wachezaji 12 ni wapya ambao ni Oswald Issa, Samir Said, Emmanuel Maganga, Ally Mohamed, Kudra Omary, Said Fundikira, Mrisho Said, Idd Kipagule, Mohamed Omary, Yohana Kimburu na Msafiri Abdallah.
Amewataja wachezaji wa zamani 14 watakaoendelea kuitumikia klabu hiyo kuwa ni pamoja na Anthony Mwingira, Eliuta Ndunguru, Bahati Yussuf, Gerarrd Mbena, Abdallah Aus, Ditram Nchimbi, Filoteus Mahundi, Mpoki Mwakinyuke, Alex Zegega, Sadiq Gawaza, Odo Nombo, Frank Sekule, Marcel Boniventure na Freddy Mbuna.