BARAZA la mitihani la taifa Nekta, limetangaza matokeo ya mitihani ya darasa la saba mwaka huu, ambapo kiwango cha ufaulu kimeongezeka kutoka asilimia 50 nukta sita moja ya mwaka jana hadi kufikia asilimia 56, nukta tisa, tisa mwaka huu.

Watahiniwa waliofanya mitihani ya kumaliza elimu ya msingi mwaka huu walikuwa ni zaidi ya laki saba na 92, elfu sawa na asilimia 98, ya watahiniwa waliosajiliwa kufanya mitihani hiyo.