Wednesday, November 5, 2014

BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA NEKTA LATANGAZA MATOKEO YA DARASA LA 7 UFAULU WAONGEZEKA.

BARAZA la mitihani la taifa Nekta, limetangaza matokeo ya mitihani ya darasa la saba mwaka huu, ambapo kiwango cha ufaulu kimeongezeka kutoka asilimia 50 nukta sita moja ya mwaka jana hadi kufikia asilimia 56, nukta tisa, tisa mwaka huu.
Akitangaza matokeo hayo jijini Dar-es-Salaam katibu mtendaji wa Nekta Dokta Chazi Msonde amesema shule za kanda ya ziwa zinaongoza ambapo shule nane kati ya kumi bora zinatoka kanda hiyo, huku mbili zilizosalia ni kutoka mkoa wa Dar-es- Salaam na Kilimanjaro.
Watahiniwa waliofanya mitihani ya kumaliza elimu ya msingi mwaka huu walikuwa ni zaidi ya laki saba na 92, elfu sawa na asilimia 98, ya watahiniwa waliosajiliwa kufanya mitihani hiyo.