Wednesday, November 5, 2014

WAZIRI NYALANDU ASEMA VITENDO VYA UJANGILI VISIPODHIBITIWA TAIFA LITAANGAMIA.

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amesema vitendo vya ujangili dhidi ya wanyama wakiwamo tembo, mbali na kuonekana kupungua nchini, lakini kasi yake isipodhibitiwa, taifa  litaangamia.
Waziri Nyalandu ametoa tahadhari hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa kitaifa uliowashirikisha viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini na wadau wa maendeleo kuhusu kujadili namna ya kudhibiti uharibifu dhidi ya rasilimali za nchi zikiwamo wanyama na misitu, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Waziri Nyalandu,amesema  kukithiri kwa vitendo hivyo kunachangiwa na madai ya kuongezeka kwa soko haramu la rasilimali za nchi zikiwamo nyara za serikali katika nchi za Vietnam, Japan, Korea, China na Thailand.
Hata hivyo Nyalandu amewataka  watu wote wanaomiliki silaha kinyume na sheria zikiwamo silaha aina ya gobore, kuzisalimisha haraka kwa hiari, vinginevyo watakumbwa na operesheni ya nyumba kwa nyumba na kuwalazimu wahusika kuchukuliwa hatua kali za kisheria.