Tuesday, December 2, 2014

CAF YAWEKA HADHARANI MAJINA YA TIMU SPECHO KWA DROO KUPANGWA.

WASHIRIKI 16 wa Fanali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, ambazo zitachezwa huko Nchini Equatorial Guinea kuanzia Januari 17, watajua nani Wapinzani kwenye Makundi yao Leo Jumatano makundi ya Timu 4 kila moja kutajwa kwa ajili ya Droo hiyo na CAF.
Droo hiyo itafanyika Mjini Malabo Nchini Equatorial Guinea.
Timu hizo 16 zimepangwa kwenye Vyungu Vinne vya Timu 4 kila moja na kwenye Droo kila Chungu kitatoa Timu moja ili kupanga Makundi Manne.
CHUNGU 1
Equatorial Guinea, Ghana, Zambia, Burkina Faso
CHUNGU 2
Ivory Coast, Mali, Tunisia, Algeria
CHUNGU 3
Cape Verde, South Africa, Gabon, DR Congo
CHUNGU 4
Cameroon, Senegal, Guinea, Congo