Timu Polisi ya Morogoro na
Mwadui FC ya Shinyanga zimewasilisha barua kumuomba beki wa pembeni Miraj Adam
wa Simba SC kwa mkopo baada ya kushushwa Simba B.
Polisi ya Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania i napambana na Mwadui FC, inayopigania kupanda Ligi Kuu pia
kuwania huduma za beki huyo aliyetokea timu ya vijana ya Wekundu hao wa
Msimbazi.
Mwadui wanaamini wanaweza
kumpata kwa urahisi beki huyo kwa sababu ya mahusiano mazuri ya kocha wao,
Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ na klabu ya Simba SC.

Kwa sasa, Miraj ameshushwa
kikosi cha pili baada ya mechi saba za awali za Ligi Kuu, lakini Simba SC bado
haijaamua kumtoa kwa mkopo hadi hapo itakapofanikisha kusajili mchezaji
mwingine wa nafasi hiyo.