Saturday, May 11, 2013

MKONGWE WA CHELSEA LAMPARD APIGA 2 AVUNJA REKODI

Kwenye mechi ya BPL LEO g la Dakika ya 88 la Frank Lampar limeleta burudani zaidi kwa Chelsea kuibuka na ushindi wa bao2-1 dhidi ya  Aston Villa Bao na hilo ni Bao lake la 203 kwa Chelsea akiwa ameivunja Rekodi ya Bobby Tambling ya Magoli 202 iliyowekwa kati ya 1959 na 1970.
Katika mchezo huu kila timu ilimaliza ikiwa Mtu 10 baada ya Ramires wa Chelsea na Christian Benteke kutolewa kwa Kadi Nyekundu.

wachezaji hawa Wote walipewa Kadi za Njano mbili na kutolewa kwa Kadi Nyekundu kwa Ramires kutolewa Dakika ya 45 na Benteke Dakika ya 58.
MAGOLI:

Aston Villa 1

Benteke Dakika ya 14

Chelsea 2
Lampard Dakika ya 61 & 88
BPL: BARCLAYS PREMIER LEAGUE

RATIBA
Jumapili Mei 12

[Saa 9 na Nusu Mchana]

Stoke v Tottenham

[Saa 11 Jioni]

Everton v West Ham

Fulham v Liverpool

Norwich v West Brom

QPR v Newcastle

Sunderland v Southampton

[Saa 12 Jioni]

Man United v Swansea

Jumanne Mei 14

[Saa 3 Dak 45 Usiku]

Arsenal v Wigan

[Saa 4 Usiku]

Reading v Man City

Jumapili 19 Mei

MECHI ZA MWISHO ZA LIGI MSIMU HUU

[Saa 12 Jioni]

Chelsea v Everton

Liverpool v QPR

Man City v Norwich

Newcastle v Arsenal

Southampton v Stoke

Swansea v Fulham

Tottenham v Sunderland

West Brom v Man United

West Ham v Reading

Wigan v Aston Villa
MSIMAMO:  BPL
PositionTeamPlayedGoalDifferencePoints
No movement1Man Utd364285
No movement2Man City363175
No movement3Chelsea373572
No movement4Arsenal363167
No movement5Tottenham361866
No movement6Everton361460
No movement7Liverpool362555
No movement8West Brom36048
No movement9Swansea36046
No movement10West Ham36-843
No movement11Stoke36-1041
No movement12Fulham36-1140
No movement13Aston Villa37-2240
No movement14Southampton36-1139
No movement15Sunderland36-1238
No movement16Norwich36-2238
No movement17Newcastle36-2338
No movement18Wigan36-2335
No movement19Reading36-2628
No movement20QPR36-2825

FAINALI YA FA CUP DIMBANI MAN CITY VS WIGAN ATHLETIC LEO

FAINALI YA FA CUP  hii leo man city mabingwa wa BPL msimu uliopita, man city wanaingia dimbani huku wakikumbuka kupokonywa taji lao la BPL na man united, na kutolewa katika michuano ya  UEFA championz ligi  katika hatua za makundi hivyo wamebakisha FA CUP tu ambapo wataumana uso kwa uso na timu ngumu ya  wigan athletic ambayo ipo hatarini kushuka daraja endapo man city wataibuka na ushindi basi  watakuwa wamemnusuru Meneja wao Roberto Mancini.
Kwa upande Man City ni Fainali ya 10 ya FA CUP na kwa upande wa  Wigan ni Fainali ya 1 tangu Timu yao ianzishwe Mwaka 1932.
FAINALI FA CUP
MUDA: SAA 1 NA ROBO USIKU LEO
UWANJA: WEMBLEY
MAN CITY VS WIGAN ATHLETIC

HARAKATI HADI KUFIKA FAINALI.
WIGAN:
-Raundi ya 3: Wigan 1 Bournemouth 1 MARUDIANO :Bournemouth 0 Wigan 1
-Raundi ya 4: Macclesfield Town  0 Wigan 1
-Raundi ya 5: Huddersfield Town 1 Wigan 4
-Raundi ya 6: Everton 0 Wigan 3
-NUSU FAINALI [Wembley]: Millwall 0 Wigan 2
MAN CITY:
-Raundi ya 3: Man City 3 Watford 0
-Raundi ya 4: Stoke City 0 Man City 1
-Raundi ya 5: Man City 4 Leeds United 0
-Raundi ya 6: Man City 5 Barnsley 0
-NUSU FAINALI [Wembley]: Man City2 Chelsea 2
Ukitoa tathimini ya haraka haraka Kwa Man City hii ni Mechi rahisi kwa upande wao kutokana wanakutana na timu kibonde Wigan Athletic ambayo katika Ligi, BPL,Barclays Premier League ipo katika janga la  kushusuhwa Daraja.
Man city fa cup wametwaa mara 5 na hii ni  fainali mara 10
Mwaka 1904, 1934, 1956, 1969 na 2011.
Kwa upande wa  Man United wamekuwa Washindi wa Pili mara 4 katika FA CUP  ambapo ni  Miaka ya 1926, 1933, 1955 na 1981.
WOTE WAWILI MATOKEO MECHI ZAMWISHO:
2012/2013
17 Apr Man City 1 Wigan 0
28 Nov Wigan 0 Man City 2
2011/2012
16 Jan Wigan 0 Man City 1
10 Sep Man City 3 Wigan 0
2010/2011
05 Mar Man City 1 Wigan 1
19 Sep Wigan 0 Man City 2
2009/2010
29 Mar Man City 3 Wigan 0
18 Okt Wigan 1 Man City 1

TIMU MBILI ZAIDI ZAPETA LIGI YA MABINGWA MKOA "RCL"

WAKATI Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaanza kutimua vumbi keshokutwa (Mei 12 mwaka huu), timu mbili zinakwenda moja kwa moja raundi inayofuata baada ya mabingwa wa Pwani, Kiluvya United kuondolewa na mkoa wa Manyara kutowasilisha bingwa wake.
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana leo (Mei 10 mwaka huu) imeiondoa Kiluvya United baada ya kubaini kuwa timu hiyo haikushiriki ligi ya mkoa wala wilaya msimu uliopita, hivyo kutokuwa na sifa ya kucheza Ligi ya Mkoa msimu huu.
Hivyo Friends Rangers ya Dar es Salaam iliyokuwa icheze na Kiluvya United na Mpwapwa Stars ya Dodoma iliyokuwa iwakabili mabingwa wa Manyara zinakwenda moja kwa moja raundi ya pili.
Timu nyingine iliyokwenda moja kwa moja raundi ya pili itakayochezwa kati ya Mei 25 na 25 mwaka huu na mechi za marudiano ni kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu baada ya kupita kwenye upangaji ratiba ni mabingwa wa Shinyanga, Stand United FC.
Kamati hiyo iliyokutana chini ya uenyekiti wa Blassy Kiondo pia imeagiza viongozi wa mikoa ya Manyara na Pwani waandikiwe barua za onyo kwa kushindwa kuwasilisha majina ya mabingwa wao.
Vilevile imesisitiza viwanja vitakavyotumika kwa mechi za RCL ni vya makao makuu ya mikoa tu, isipokuwa kwa Uwanja wa CCM Mkamba ulioko Ifakara, Morogoro ambao ulishakaguliwa na TFF, hivyo kutumika kwa michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu. Pia usajili unaotumika katika RCL ni ule ule wa ligi ya mkoa.
Mechi za Mei 12 mwaka huu zitakuwa kati ya Kariakoo ya Lindi dhidi ya Coast United ya Mtwara (Uwanja wa Ilulu), Techfort ya Morogoro vs African Sports ya Tanga (Uwanja wa CCM Mkamba), Machava FC ya Moshi vs Flamingo SC ya Arusha (Uwanja wa Ushirika), Simiyu United ya Simiyu vs Magic Pressure ya Singida (Uwanja wa Simiyu) na Polisi Jamii Bunda ya Mara vs UDC ya Mwanza (Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume).
Polisi SC ya Geita vs Biharamulo FC ya Kagera (Uwanja wa Geita), Saigon FC ya Kigoma vs Milambo FC ya Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika), Katavi Warriors ya Katavi vs Rukwa United ya Rukwa (Uwanja wa Katavi), Njombe Mji ya Njombe vs Mbinga United ya Ruvuma (Uwanja wa Sabasaba) na Kimondo SC ya Mbeya dhidi ya 841 KJ FC ya Iringa (Uwanja wa Sokoine, Mbeya).
Mechi kati ya Red Coast na Abajalo itachezwa Mei 13 mwaka huu Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam. Mei 12 mwaka huu uwanja huo utatumika kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Azam na Mgambo Shooting.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Friday, May 10, 2013

YANGA CHATUA VISIWANI PEMBA KUJIWEKA SAWA KUFUTA KIPIGO CHA 5-0

Wanandinga wa jangwani  Yanga SC wamewasili kisiwani Pemba kuweka kambi ya kujiandaa na mtanange mkali dhidi ya wapinzani wao wa jadi, Simba SC Mei 18,  katika dimba la Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
wanajangwani hao watakuwa huko hadi siku moja kabla ya mechi itakaporejea  jijini Dar es Salaam.

Pamoja na kuwa  Yanga tayari imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu, lakini imeipa uzito mkubwa mechi hiyo kwa sababu inataka kulipa kisasi cha kufungwa 5-0 na wapinzani wao hao wa jadi mwaka jana.
Tangu utawala mpya  uingia madarakani, uongozi wa Yanga chini ya Mwenyekiti, Alhaj Yussuf Mehboob Manji umekuwa ukiumia kichwa na kipigo cha 5-0 mwaka jana.

Mara kadhaa Manji amewahi kukaririwa  akisema kwamba 5-0 zinamuumiza kichwa hasa katika wakati ambao idadi ya mabao katika mechi za timu hiyo ilipungua.
Kihistoria, Simba SC imewahi kuipa Yanga vipigo viwili vitakatifu 6-0 mwaka 1977 na 5-0 mwaka jana, wakati Yanga iliifunga SImba 5-0 mwaka 1969.  
Safari hii, Yanga imepania kuweka heshima kwa kuhakikisha inaitwangwa simba kwa  kipigo kitakatifu  na kuvunja rekodi ya 6-0 ya vipigo hivyo.


IFAHAMU KWA UNDANI ZAIDI YANGA KATIKA HARAKATI ZASOKA"

JINA KAMILI :Young  afrikani Sports Club
ILIANZISHWA : mwaka 1935
KOCHA: Ernie Brandts
LIGI: Ligi Kuu ya Tanzania bara
LIGI KUU TANZANIA:  Mara 24
1968, 1969, 1970, 1971, 1972, 1974, 1981, 1983, 1985, 1987, 1989, 1991, 1992, 1993, 1996, 1997, 1998, 2002, 2005, 2006, 2008, 2009, 2011,2013
TANZANIA KOMBE  : Mara 4
1975, 1994, 1999, 2000.
CECAFA CLUB KOMBE / KAGAME INTERCLUB KOMBE:  Mara 5
Mwaka : 1975, 1993, 1999, 2011, 2012
UTENDAJI KATIKA MASHINDANO YA CAF   SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU AFRIKA:
CAF LIGI YA MABINGWA: KUSHIRIKI  MARA 8
1997 - Raundi ya mchujo
1998 - Hatua ya makundi
2001 - Raundi ya Pili
2006 - Raundi ya mchujo
2007 - Raundi ya Pili
2009 - Raundi ya kwanza
2010 - Raundi ya mchujo
2012 - Raundi ya mchujo
KOMBE LA MABINGWA WA KLABU: 11 KUSHIRIKI
1969 - Robo Fainali
1970 - Robo Fainali
1971 - aliondoka katika raundi ya pili
1972 - Raundi ya kwanza
1973 - Raundi ya kwanza
1975 - Raundi ya Pili
1982 - Raundi ya Pili
1984 - Raundi ya kwanza
1988 - Raundi ya kwanza
1992 - Raundi ya kwanza
1996 - Raundi ya mchujo
KOMBE LA SHIRIKISHO LA CAF: 3 KUONEKANA
2007 – Raundi ya  mzunguuko wa  kati
2008 - Raundi ya kwanza
2011 - Raundi ya mchujo
CAF KOMBE: 2 KUONEKANA
1994 - Raundi ya kwanza
1999 - Raundi ya kwanza
Kombe la CAF la washindi: 2 kuonekana
1995 - Robo Fainali
2000 - Raundi ya kwanza