Sunday, May 12, 2013

MFAHAMU ZAIDI MICHAEL ESSIEN KATIKA ULIMWENGU WA KANDANDA"

                               Michael Essien
Essien Real Madrid.JPG
Taarifa kuhusu yeye
Full nameMichael Kojo Essien
Date of birth3 December 1982 (age 30)
Place of birthAccraGhana
Height1.77 m (5 ft 10 in)[2]
Playing positionMidfielder
Timu ya sasa
Current clubReal Madrid
(on loan from Chelsea)
Number15
Youth career
1999–2000Liberty Professionals
Senior career*
mwakaTimuMechi(Goli}
2000–2003Bastia66(11)
2003–2005Lyon71(7)
2005–Chelsea163(17)
2012–→ Real Madrid (loan)18(1)
Timu ya taifa
2002–Ghana52(9)


MATAJI AKIWA NA CLUB HIZI
Lyon
Ligue 1 (2): 2003-04, 2004-05
Trophée des Mabingwa (2): 2003, 2004
Chelsea
Ligi Kuu (2): 2005-06, 2009-10
Kombe la FA (4): 2006-07, 2008-09, 2009-10, 2011-12
Kombe la Ligi (1): 2006-07
FA Community Shield (1): 2009
Ligi ya Mabingwa (1): 2011-12

TUZO BINAFSI
2005 UNFP Ligue 1 Mchezaji wa Mwaka
BBC Afrika Mchezaji wa Mwaka: 2006 [56]
Ghana Mchezaji wa mwaka: 2008
Lengo la Chelsea msimu: 2006-07 vs Arsenal, [57]
2008-09 vs Barcelona [57]
2008 Kombe la Mataifa ya Timu ya mashindano [58]
Chelsea Mchezaji wa Mwaka: 2007 [57]
Ligue 1 Timu ya Mwaka: 2003
Ligue 1 Timu ya Mwaka: 2005

AZAM FC YAITANDIKA JKT MGAMO 3-0 KUCHEZA KOMBE LA SHIRIKISHO

AZAM FC imefanikiwa rasmi kucheza michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Mgambo Shooting jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Ushindi huo, unaifanya Azam ifikishe pointi 51, nne nyuma ya mabingwa, Yanga SC wenye 57 kila timu ikiwa imebakiza mechi moja kumaliza ligi.

Hadi mapumziko, tayari Azam FC walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na John Raphael Bocco dakika ya 23 kufuatia kazi nzuri9 ya Humphrey Ochieng Mieno.
Kipindi cha pili, Azam tena walirudi na kasi nzuri na kufanikiwa kupata bao la pili dakika ya 65 lililofungwa na Kipre Herman Tchetche baada ya kuichambua ngome ya wapinzani na kupioga shuti mariadi.
Hilo lilikuwa bao lake la 17 msimu huu hivyo kujihakikishia ufungaji bora wa Ligi Kuu, akiritihi mikoba ya Bocco ‘Adebayor’, ambaye naye alimrithi Mrisho Khalfan Ngassa akiwa Azam pia kabla ya kutolewa kwa mkopo Simba SC.  
Joackins Otieno Atudo aliunganishwa kwa kichwa kona ya Erasto Edward Nyoni dakika ya 80 na mpira ukatinga nyavuni na hata kipa Tonny Kavishe alipojaribu kuuokolea ndani, lakini ukagonga nyavu za juu na kudondokea ndani tena, hilo likiwa bao la tatu katika mchezo wa leo.
Azam sasa watacheza tena michuano ya Shirikisho mwakani, baada ya mwaka huu kutolewa Raundi ya Tatu na AS FAR Rabat ya Morocco wakishiriki kwa mara ya kwanza.

VIKOSI VYA TIMU ZOTE MBILI
Mwadini Ally, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Aggrey Morris, Joackins Atudo, Kipre Balou/Ibrahim Mwaipopo dk85, Kipre Tchetche, Salum Abubakar, John Bocco, Humprey Mieno/Abdi Kassim dk83 na Brian Umony/Seif Abdallah dk63. 
JKT Mgambo; Tony Kavishe, Salum Mlima, Ramadhani Malima, Bashiru Chanacha, Bakari Mtama, Salum Kipanga, Mussa Gunda, Juma Mwinyimvua/Peter Mwalyanzi dk 56, Issa Kandulu, Fully Maganga na Nassor 
Gumbo.

 RATIBA.
Jumamosi Mei 18
Toto Africans Vs Ruvu Shooting
Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
Simba SC Vs Yanga SC
JKT Oljoro Vs Azam FC
Polisi Moro Vs Coastal Union
MSIMAMO:
KUMBUKA YANGA BINGWA
NA
TIMU
P
W
D
L
GF
GA
GD
PTS
1
YANGA
25
17
6
2
45
14
31
57
2
AZAM FC
25
14
6
4
42
20
25
51
3
SIMBA SC
25
12
9
4
38
23
15
45
4
KAGERA SUGAR
25
11
7
6
25
18
8
41
5
MTIBWA SUGAR
25
10
9
6
29
24
5
39
6
COASTAL UNION
25
8
11
6
25
23
2
35
7
RUVU SHOOTING
25
8
7
9
21
23
-2
32
8
JKT OLJORO
25
7
8
10
21
26
-5
29
9
TANZANIA PRISONS
25
7
8
10
16
22
-6
29
10
JKT RUVU
25
7
5
13
21
38
-17
26
11
MGAMBO SHOOTING
25
7
4
13
16
24
-8
25
12
POLISI MOROGORO
25
4
10
11
13
23
-10
22
13
TOTO AFRICAN
25
4
10
11
21
33
-12
22
14
AFRICAN LYON
25
5
4
16
16
38
-22     
19

Saturday, May 11, 2013

FA CUP: WIGAN MABINGWA, MAN CITY HOI HATA KOMBE MOJA MSIMU HUU


Kunako dakika ya  91 goli la Ben Watsoni  limewapa ubingwa Wigan athletic, Timu ambayo ipo katika janga la  kushushwa Daraja, wa Bao 1-0 walipoitandika Manchester City kwenye Fainali ya FA CUP  iliyopigwa katika dimba la Wembley Stadium hii leo.
katika mtanange wa leo wigan  Wigan walionekana  kuonyesha bora na  ushirikiano mzuri sana huku Mchezaji wao Callum McManaman akiwatesa sana na kusababisha   Pablo Zabaleta wa city kutolewa nje kwa kupewa Kadi ya Njano ya Pili na hivyo kuzawadiwa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 83.
shangwe na nderemo hii kubwa  wigan utwaa Taji lao la kwanza katika Histora yao Wigan wana kibarua kigumu kujihakikishia wanaepukana na janga la kushushwa Daraja kwani wapo katka nafasi ya 3 toka mkiani na wamebakisha Mechi 2 tu, ya kwanza ikiwa ni Jumanne Uwanjani Emirates watakapoivaa Arsenal.
WASHINDI WA FA CUP
FA_CUP-NEW_LOGO
2013
wigan athletic
2012
Chelsea FC
2011
Manchester City
2010
Chelsea FC
2009
Chelsea FC
2008
Portsmouth FC
2007
Chelsea FC
2006
Liverpool FC
2005
Arsenal FC
2004
Manchester United
2003
Arsenal FC
2002
Arsenal FC
2001
Liverpool FC
2000
Chelsea FC
1999
Manchester United
1998
Arsenal FC
1997
Chelsea FC
1996
Manchester United
1995
Everton FC
1994
Manchester United
1993
Arsenal FC
1992
Liverpool FC
1991
Tottenham Hotspur
1990
Manchester United
1989
Liverpool FC
1988
Wimbledon FC
1987
Coventry City
1986
Liverpool FC
1985
Manchester United
1984
Everton FC
1983
Manchester United
1982
Tottenham Hotspur
1981
Tottenham Hotspur
1980
West Ham United
1979
Arsenal FC
1978
Ipswich Town
1977
Manchester United
1976
Southampton FC
1975
West Ham United
1974
Liverpool FC
1973
Sunderland AFC
1972
Leeds United
1971
Arsenal FC
1970
Chelsea FC
1969
Manchester City
1968
West Bromwich Albion
1967
Tottenham Hotspur
1966
Everton FC
1965
Liverpool FC
1964
West Ham United
1963
Manchester United
1962
Tottenham Hotspur
1961
Tottenham Hotspur
1960
Wolverhampton Wanderers
1959
Nottingham Forest
1958
Bolton Wanderers
1957
Aston Villa
1956
Manchester City
1955
Newcastle United
1954
West Bromwich Albion
1953
Blackpool FC
1952
Newcastle United
1951
Newcastle United
1950
Arsenal FC
1949
Wolverhampton Wanderers
1948
Manchester United
1947
Charlton Athletic
1946
Derby County
1939
Portsmouth FC
1938
Preston North End
1937
Sunderland AFC
1936
Arsenal FC
1935
Sheffield Wednesday
1934
Manchester City
1933
Everton FC
1932
Newcastle United
1931
West Bromwich Albion
1930
Arsenal FC
1929
Bolton Wanderers
1928
Blackburn Rovers
1927
Cardiff City
1926
Bolton Wanderers
1925
Sheffield United
1924
Newcastle United
1923
Bolton Wanderers
1922
Huddersfield Town
1921
Tottenham Hotspur
1920
Aston Villa
1915
Sheffield United
1914
Burnley FC
1913
Aston Villa
1912
Barnsley FC
1911
Bradford City
1910
Newcastle United
1909
Manchester United
1908
Wolverhampton Wanderers
1907
Sheffield Wednesday
1906
Everton FC
1905
Aston Villa
1904
Manchester City
1903
Bury FC
1902
Sheffield United
1901
Tottenham Hotspur
1900
Bury FC
1899
Sheffield United
1898
Nottingham Forest
1897
Aston Villa
1896
Sheffield Wednesday
1895
Aston Villa
1894
Notts County
1893
Wolverhampton Wanderers
1892
West Bromwich Albion
1891
Blackburn Rovers
1890
Blackburn Rovers
1889
Preston North End
1888
West Bromwich Albion
1887
Aston Villa
1886
Blackburn Rovers
1885
Blackburn Rovers
1884
Blackburn Rovers
1883
Blackburn Olympic
1882
Old Etonians
1881
Old Carthusians
1880
Clapham Rovers
1879
Old Etonians
1878
The Wanderers
1877
The Wanderers
1876
The Wanderers
1875
Royal Engineers
1874
Oxford University
1873
The Wanderers
1872
The Wanderers
WALIOTWAA MARA NYINGI FA CUP:
Man United Mara 11
Arsenal 10
Tottenham Hotspur 8
Liverpool 7
Chelsea  7
Aston Villa 7
Newcastle United 6
Blackburn Rovers 6
Everton 5
West Bromwich Albion 5
Manchester City 5
Bolton Wanderers 5  

MABINGWA WA LIGI KUU VODACOM TZ BARA KUJIPATIA MIL.200 MSIMU HUU


MDHAMINI wa Ligi Kuu Tanzana Bara inayofikia tamati mei 18 mwaka huu, Kampuni ya Vodacom imetangaza kutumia kiasi cha Shilingi Mil 200 kwa ajili ya kutoa zawadi ya fedha taslimu katika ligi inayomalizika mei 18 ambapo sasa Mabingwa wa msimu huu watajipatia Shilingi Milioni 70.

Mbali ya bingwa, Vodacom pia itatoa fedha kwa timu inayomaliza nafasi ya pili, ya tatu na  ya nne katika msimamo wa ligi ambazo ni Sh. 35 Milioni,  huku Sh. 25 Milioni na Sh. 20 Milioni zote zikiwa na ongezeko ikilinganishwa na zawadi za fedha zilizotolewa katika msimu wa 2012 / 2013.

Zawadi hizo zimetangazwa kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kampuni hiyo kupitia Meneja Uhusiano wa Mambo ya Nje wa Vodacom Salum Mwalim, ikiwa ni pamoja na kuainisha zawadi za washindi wa mchezaji mmoja mmoja pamoja na timu iliyoonyesha nidhamu kwa msimu huu.

"Mwaka huu tutatumia kiasi cha Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya zawadi za fedha taslimu kwa  washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom huku bingwa akinyakua kitita cha Shilingi Milioni 70 ikilinganishwa na Sh 50 Milioni za msimu uliopita." Alisema Mwalim.

Mwalimu amesema lengo la kuongeza zawadi ni matokeo ya ushirikiano mzuri kati ya wadhamini wa ligi na wadau wengine wa soka na kwa pamoja kuwa na dhamira ya dhati katika kuendeleza soka nchini.
"Kila mmoja ni shahidi wa namna ambavyo soka letu limekuwa na namana ambavyo tunakabaliana hatua kwa hatua na changamoto zinazohusiana na ligi. Ni matumaini yetu kwamba tunapiga hatua na tuna matumaini ya kufikia kiwango cha juu zaidi cha maendeleo ya soka nchini yanaonekana." Aliongeza Mwalim "Kwetu sisi kama wadhamini tutajitahidi kadri inavyowezekana kuhakiksha tunaleta mabadiliko katika soka la Tanzania, tunaangalia mpira wa miguu nchini kwa upana zaidi kama mchezo unaopendwa, unaotuleta pamoja kama taifa na kuitangaza nchi yetu. Falsafa yetu hii imechangia kwa kiasi kikubwa kuwepo utulivu na ushirikiano mzuri miongoni mwa wadau na hivyo kutuletea mafanikio." Alisema Mwalim Zawadi nyingine zilizo tangazwa ni pamoja na zawadi ya mchezaji bora wa Mwaka golikipa bora, na mfugaji bora kila mmoja  anajinyakulia Shilingi Milioni 5.
Aidha, mwamumzi bora na kocha bora kila mmoja atajipatia Shilingi 7,500,000 kila huku timu iliyoongoza kwa nidhamu itapata zawadi ya fedha taslimu ya Shilingi Milioni 15.
"Tumekuwa na msimu mzuri uliojaa ushindani na hamasa, tunatarajia timu zitajipanga zaidi kwa ajili ya msimu ujao na hivyo kuendelea kuipa ubora ligi yetu."Alisema Mwalim huku akiwashukuru wadau wa mpira wa miguu nchini ikiwemo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Bodi ya Ligi, Chama cha Waamuzi(FRAT), Vilabu, wachezaji na kipekee washabiki na kamati ya ligi kuu.
Amesema bila ya ushirikiano wa wadau hao na wengine ikiwemo Serikali, ligi kuu ya Vodacom isingeweza kufikia maendeleo iliyoyafikia katika msimu unaomalizika ambao kwa kiasi kikubwa ulitawaliwa na mpira wa uwanjani na si vinginevyo.