Thursday, June 6, 2013

ETO"O ATWAA MCHEZAJI BORA WA LIGI NCHINI URUSI.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Cameroon na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi Samuel Eto’o ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa msimu wa Ligi Kuu ya nchi hiyo kwa msimu wa 2012-2013. Eto’o ambaye amewahi kunyakuwa tuzo ya mchezaji bora Afrika mara nne, alikabidhiwa tuzo hiyo baada ya kuisadia timu yake kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wan chi hiyo. Akihojiwa mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo Eto’o ambaye pia ni nahodha wa timu hiyo amedai kufurahishwa na hatua hiyo na kuwashukuru mashabiki wa soka nchini humo pamoja na waandishi wa habari kwa kuwa nyuma yake wakati wote. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 atakosa mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 wa timu ya taifa ya nchi yake dhidi ya Togo utakaochezwa Juni 9 mwaka huu kutokana na majeraha yanayomsumbua. 
SAMWELI ETO'O KATIKA ULIMWENGU WA SOKA
Samuel 2011.jpg
Eto'o in 2011.
Kuhusu yeye
Full nameSamuel Eto'o Fils
Date of birth10 March 1981 (age 32)
Place of birthDoualaCameroon[1]
Height1.80 m (5 ft 11 in)[2]
Playing positionStriker
Timu
Current clubAnzhi Makhachkala
Number9
academy
1992–1997Kadji Sports Academy
Timu za ukubwa
YearsTeammechi(Goli)"
1997–2000Real Madrid3(0)
1997–1998→ Leganés (mkopo)30(4)
1999→ Espanyol (mkopo)0(0)
2000→ Mallorca (mkopo)19(6)
2000–2004Mallorca120(48)
2004–2009Barcelona145(108)
2009–2011Internazionale67(33)
2011–Anzhi Makhachkala43(21)



SPAIN BADO NAMBA MOJA UBORA DUNIANI - FIFA

Mabingwa wa Dunia timu ya taifa ya Spain bado ndio inaendelea kushika namba moja katika Listi ya viwango vya FIFA vya Ubora Duniani iliyotolewa leo ikifuatiwa na timu ya taifa ya ujerumani ambapo nafasi ya tatu inashikiliwa na  Argentina  ambapo nafasi ya nne ikishikiliwa na  Croatia, huku Tanzania Taifa star ikipanda Nafasi 7 kutoka 116 hadi 109.
Katika 10 Bora, Netherlands imepanda  mpaka Nafasi ya 5, Portugal kushuka Nafasi moja hadi ya 6, Colombia, wameshuka Nafasi 2 na wapo nafasi ya 7 huku timu ya taifa ya England ikiporomoka Nafasi 2 na sasa wako Nafasi ya 9.
Kwa Nchi za Afrika, Côte d'Ivoire ndio ipo Nafasi ya juu kabisa ikiwa Nafasi ya 13 ikifuatiwa na Ghana iliyokatika Nafasi ya 20.
Brazil, ambayo imeathirika kwa kucheza Mechi za Kirafiki tu kwa Miaka miwili, imeporomoka Nafasi 2  hadi Nafasi ya 22 lakini kushiriki kwao katika Mashindano rasmi ya FIFA ya kugombea Kombe la Mabara yatakayochezwa Nchini brazil  kuanzia Juni 15 kama watafanya vizuri basi itawaletea faida nzuri na sana katika harakati za kupanda chati.
Toleo jingine la Listi ya FIFA ya Ubora Duniani litatolewa Julai 4.
25 BORA:
1        Spain
2        Germany
3        Argentina
4        Croatia
5        Netherlands
6        Portugal
7        Colombia
8        Italy
9        England
10      Ecuador
11      Russia
12      Belgium
13      Côte d'Ivoire
14      Switzerland
15      Bosnia-Herzegovina
16      Greece
17      Mexico
18      France
19      Uruguay
20      Denmark
21      Ghana
22      Brazil
23      Mali
24      Czech Republic
25      Chile
NCHI ZINAZOIZUNGUKA TANZANIA:
104    Qatar
105    Lithuania
106    Ethiopia
107    Niger
108    Saudi Arabia
109    Malawi
109    Tanzania {imepanda nafasi 7]
111    Kuwait
112    Tajikistan
113    Suriname
114    Korea DPR
115    Benin 308
116    Northern Ireland

JESUS AONGEZEWA MKATABA MPYA NDANI YA KLABU YA BENFICA.


KLABU ya Benfica ya Ureno imetangaza kumuongezea mkataba mpya kocha wake Jorge Jesus atakao dumu nao klubuni hapo mpaka katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka 2015. Kulikuwa na wasiwasi kama kocha huyo mwenye umri wa miaka 58 anaweza kubakia katika klabu hiyo baada ya kumaliza msimu na kuambulia patupu. Hata hivyo Jesus sasa amemaliza utata huo kwa kusaini miaka miwili zaidi na klabu hiyo inayotoka katika jijini Lisbon. Jesus alianza kuinoa Benfica kuanzia mwaka 2009 na kuingoza kushinda taji moja la Ligi Kuu na matatu ya Kombe la Ligi la nchi hiyo.

PEREZ. AWEKA WAZI KUWA ZIDANE HANA UZOEFU WA KUTOSHA KUWA KOCHA.

Florentino Perez rais wa klabu ya Real Madrid ametanabaisha na kusema kuwa Zinedine Zidane ana vigezo vyote vinavyohitajika kuchukua nafasi ya Jose Mourinho lakini anadhani bado anahitaji uzoefu zaidi kabla ta kukabidhiwa mikoba hiyo. Perez amesema Zidane ana kila kitu ambacho kocha anatakiwa kuwa nacho na kazi hiyo anaiweza lakini bado anahitaji uzoefu ili kukabidhiwa majukumu makubwa kama hayo. Kwasasa chaguo la kwanza la Madrid katika kutafuta mbadala wa Mourinho ni kocha wa Paris Saint-Germain Carlo Ancelotti ingawa Perez alishindwa kuliongelea kwa kuogopa kuwachukiza PSG ambao bado wamemng’ang’ania kocha huyo. Zidane ambaye ameichezea Madrid kuanzia mwaka 2001 mpaka 2006 kwasasa ni mkurugenzi wa michezo na kocha wa vijana wa klabu hiyo.


      WASIFU WA  ZIDANE
Zinedine Zidane 2008.jpg
Taarifa kuhusu yeye
Full name
Zinedine Yazid Zidane
Date of birth
23 June 1972 (age 40)
Place of birth
Marseille, France
Height
1.85 m (6 ft 1 in)
Playing position
Timu za Ujana
1982–1983
US Saint-Henri
1983–1986
SO Septèmes-les-Vallons
1986–1989
Timu za Ukubwa
Mwaka
Timu
Mechi
Goli
1989–1992
61
(6)
1992–1996
139
(28)
1996–2001
151
(24)
2001–2006
155
(37)
Total
506
(95)
Timu ya Taifa
1988–1989
4
(1)
1989–1990
6
(0)
1990–1994
20
(3)
1994–2006
108
(31)

MARTINEZ ACHUA NAFASI YA DAVID MOYES KUIFUNDISHA EVERTON.

MENEJA wa zamani wa klabu ya Wigan Athletic, Roberto Martinez ameteuliwa kuwa meneja mpya wa klabu ya Everton akichukua mikoba ilioachwa wazi na David Moyes aliyekwenda Manchester United. Martinez mwenye umri wa miaka 39 alifanikiwa kutwaa taji la Kombe la FA msimu huu, lakini aliomba kuondoka baada ya kuihakikishia timu hiyo nafasi ya kubakia katika Ligi Kuu nchini Uingereza. Mwenyekiti wa Wigan, Dave Whelan alimruhusu kocha huyo raia wa Hispania kuondoka na tayari wako katika mchakato wa kutafuta kocha mwingine wa kuziba pengo hilo. Martinez ambaye pia amewahi kuinoa Swansea City alijiunga na Wigan Juni mwaka 2009 na Aston Villa walitaka kumchukua mwaka 2011 lakini aliamua kubakia Wigan mpaka msimu huu alipoamua kuelekea Everton.

Tuesday, June 4, 2013

PEREZ AWEKA WAZI KUWA RONALDO ATABAKI REAL MADRID"

Florentino Perez rais wa club ya Real Madrid ametanabaisha kuwa ana mategemeo kuwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Cristiano Ronaldo atabakia Santiago Bernabeu katika kipindi chote cha maisha yake ya soka. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ureno, mapema mwaka jana alidokeza kuwa hakuwa anafurahia maisha ya Madrid na toka wakati huko amekuwa akihusishwa na mpango wa kurejea Manchester United pamoja na Paris Saint-Germain-PSG. Lakini Perez amedai kuwa atafanya kila awezalo ili nyota huyo aweze kuwa na furaha katika klabu hiyo na kumalizika muda wake wa kucheza soka akiwa hapo. Perez pia aluzungumzia mustakabali ya mshambuliaji mwingine Gonzalo Higuain na kudai kuwa hakuna yoyote aliyemwambia kwamba mchezaji huyo ataondoka kwani klabu hiyo haijamuweka sokoni katika kipindi cha usajili. Ambapo aliongeza kuwa kama mchezaji mwenyewe ndio anataka kuondoka basi klabu itakayomhitaji itatakiwa kuwalipa lakini mpaka sasa ahkuna klabu yoyote iliyojitokeza kumtaka mchezaji huyo.

KATIKA MISUKOSUKO YA HAPA NA PALE SASA ATUA COAST"


Baada ya kupata misukosuko ya hapa na pale katika Club ya wekundu wa msimbazi SC kiungo Haruna Moshi Shaaban ‘Boban hatimaye amefanikiwa kutua  ndani ya jiji la tanga kuichezea Coastal union mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
hivyo mpaka sasa Coastal union imekamilisha usajili wa wachezaji wanne wapya, akiwemo mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Zanzibar msimu huu, Abdallah Othman Ally. 
Ally anayecheza upande wa pembeni juu kushoto mwenye speed na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira, amesaini Mkataba wa miaka miwili na Coastal Union ambayo tangu ipande tena Ligi Kuu mwaka juzi, imepania kurejesha makali yake. Mbali na Ally anayechezea pia timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes.
Wagosi wa Kaya wamemrejesha kiungo waliyemuibua mwaka 2000 kabla ya kufuata maslahi Moro United, baadaye Simba SC na Geffle FF ya Sweden’.
Boban amerejea Tanga alipoanzia kucheza soka ya ushindani mwaka 2000 chini ya kocha maarufu zamani Mansour Magram, sasa marehemu akitokea sekondari ya Makongo, Dar es Salaam.
Aidha wagosi hao pia imesajili wachezaji wawili kutoka JKT Oljoro ya Arusha, kipa Said Lubawa na sentahafu Marcus Ndehele ambapo Mwenyekiti wa  Coastal Union Hemed Aurora hmed akizungumza na mtandao huu ametanabaisha na kusema kuwa bado wanatazama harakati za kuwanasa wachezaji watano zaidi kulingana na mapendekezo ya benchi la ufundi.  

Aidha Aurora ameongeza na kusema kuwa huu ni usajili wa uliokuwa na malengo na si wa kukurupuka na pia vilevile ni usajili unaotokana na mapendekezo ya benchi la ufundi la timu chini ya kocha mkuu, Ahmed Morocco ambaye alitaka wachezaji tisa ambao aliwapendekeza kwa majina yeye mwenyewe na sisi tumekuwa tukimfuata mmoja baada ya mwingine na kumalizana naye.
Hivyo kwa wakati huu bado tupo kwenye harakati za kumalizana na wengine watano ambpo Lengo letu ni kuhakikisha kocha anakuwa na timu atakayoridhika nayo kulingana na mapendekezo yake, hatutaki kuingilia kusajili hata mchezaji mmoja, alisema Aurora.
Mbali na hilo Aurora ameudokeza mtandao huu kuwa miongoni mwa wachezaji hao waliobaki mtazamo zaidi ni kumnasa beki aliepatwa na misukosuko kama ya Boban yaani beki mwenye nguvu na na uwezo wa kukaba Juma Nyoso.

Hata hivyo Aurora ameongeza na kusema kuwa mazoezi ya Coastal Union yataanza wiki ya kwanza ya mwezi Julai mwaka huu, nje kidogo ya mji ambako kikosi kitapiga kambi kujiandaa kikamilifu kwa ajili ya msimu mpya.