Tuesday, June 4, 2013

PEREZ AWEKA WAZI KUWA RONALDO ATABAKI REAL MADRID"

Florentino Perez rais wa club ya Real Madrid ametanabaisha kuwa ana mategemeo kuwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Cristiano Ronaldo atabakia Santiago Bernabeu katika kipindi chote cha maisha yake ya soka. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ureno, mapema mwaka jana alidokeza kuwa hakuwa anafurahia maisha ya Madrid na toka wakati huko amekuwa akihusishwa na mpango wa kurejea Manchester United pamoja na Paris Saint-Germain-PSG. Lakini Perez amedai kuwa atafanya kila awezalo ili nyota huyo aweze kuwa na furaha katika klabu hiyo na kumalizika muda wake wa kucheza soka akiwa hapo. Perez pia aluzungumzia mustakabali ya mshambuliaji mwingine Gonzalo Higuain na kudai kuwa hakuna yoyote aliyemwambia kwamba mchezaji huyo ataondoka kwani klabu hiyo haijamuweka sokoni katika kipindi cha usajili. Ambapo aliongeza kuwa kama mchezaji mwenyewe ndio anataka kuondoka basi klabu itakayomhitaji itatakiwa kuwalipa lakini mpaka sasa ahkuna klabu yoyote iliyojitokeza kumtaka mchezaji huyo.