Mabingwa wa ligi kuu nchini uingereza msimu wa 2011-2012 klabu ya Manchester City imetangaza rasmi kumsajili kiungo wa kimataifa wa Brazil Fernadinho kutoka klabu ya Shakhtar Donetski ya Ukraine. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28 amekuwa katika rada za City kwa karibu msimu mzima na anajulikana nchini Uingereza kwa kuifungia klabu yake bao katika ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Chelsea katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi msimu uliopita. City ambao mpaka sasa hawajapa mbadala wa kocha Roberto Mancini aliyeondoka, hawakutoa taarifa zozote za kiasi cha fedha walizomnunulia mchezaji huyo lakini kumekuwa na tetesi katika vyombo vya habari nchini Uingereza kuwa amewagharimu kiasi cha paundi milioni 30. Akihojiwa Fernadinho amesema kuwa hayo ni mabadiliko, changamoto na nafasi aliyokuwa akiisubiria kwa kipindi kirefu na kuichezea City ni kama ndoto zake zimekuwa kweli.
Friday, June 7, 2013
FALCAO AWEKA WAZI KUWA NIA KUBWA NI KUIPA MAFANIKIO MONACO.
MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao amesema nia yake kubwa ni kuisadia klabu ya Monaco ya Ufaransa kuwa moja ya klabu bora barani Ulaya kwa mara nyingine tena. Akihojiwa baada ya mazoezi na timu yake ya taifa jana Alhamisi Falcao amesema anajisikia fahari kubwa kuwapo Monaco hivyo kutokana na kuvutiwa na mipango waliyokuwa nayo katika kipindi kijacho hivyo mategemeo yao nikuifikisha timu hiyo katika anga za mafanikio. Akiwa Monaco nyota huyo wa zamani wa klabu ya Atletico Madrid ataungana na winga James Rodriguez ambaye pia ni raia wa Colombia baada ya kukubali uhamisho akitokea klabu ya FC Porto. Falcao amesema ana mahusiano mazuri na winga huyo na sio katika soka pekee bali wamekuwa marafiki wa karibu hata nje ya uwanja, na kummwagia sifa kwamba ni mchezaji bora ndio maana Monaco wametumia fedha nyingi kumsajili.
BOLT MKALI WA MBIO FUPI DUNIANI KUKABIDHI ZAWADI NCHINI UFARANSA.

Bolt bingwa mara sita wa michuano ya Olimpiki ambaye jana alishindwa kutamba katika mashindano ya Diamond League yaliyofanyika jijini Rome itali baada ya kushindwa na Justin Gatlin wa Marekani, atakuwa mwanariadha wa kwanza kupata heshima hiyo kwenye michuano mikubwa ya tenisi.
Nusu fainali kwa upande wanaume inatarajiwa kufanyika leo ambapo bingwa mtetezi wa michuano hiyo Rafael Nadal anatarajia kuchuana na Novak Djokovic ukifuatiwa na mchezo mwingine wa nusu fainali kati ya Jo-Wilfried Tsonga dhidi ya David Ferrer. Kwa upande wa wanawake ambapo fainali itafanyika Jumamosi kati ya Serena Williams na maria Sharapova, tuzo yao itakabidhiwa na bingwa mara tatu wa zamani wa michuano hiyo ambaye pia amewahi kuongoza katika orodha za ubora kwa wanawake Arantxa Sanchez Vicario wa Hispania.
Thursday, June 6, 2013
GALLIANI ASEMA HATUNA MPANDO NA KAKA KUJA MILAN.

ETO"O ATWAA MCHEZAJI BORA WA LIGI NCHINI URUSI.
MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Cameroon na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi Samuel Eto’o ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa msimu wa Ligi Kuu ya nchi hiyo kwa msimu wa 2012-2013. Eto’o ambaye amewahi kunyakuwa tuzo ya mchezaji bora Afrika mara nne, alikabidhiwa tuzo hiyo baada ya kuisadia timu yake kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wan chi hiyo. Akihojiwa mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo Eto’o ambaye pia ni nahodha wa timu hiyo amedai kufurahishwa na hatua hiyo na kuwashukuru mashabiki wa soka nchini humo pamoja na waandishi wa habari kwa kuwa nyuma yake wakati wote. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 atakosa mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 wa timu ya taifa ya nchi yake dhidi ya Togo utakaochezwa Juni 9 mwaka huu kutokana na majeraha yanayomsumbua.
![]() Eto'o in 2011. | |||
Kuhusu yeye | |||
---|---|---|---|
Full name | Samuel Eto'o Fils | ||
Date of birth | 10 March 1981 (age 32) | ||
Place of birth | Douala, Cameroon[1] | ||
Height | 1.80 m (5 ft 11 in)[2] | ||
Playing position | Striker | ||
Timu | |||
Current club | Anzhi Makhachkala | ||
Number | 9 | ||
academy | |||
1992–1997 | Kadji Sports Academy | ||
Timu za ukubwa | |||
Years | Team | mechi | (Goli)" |
1997–2000 | Real Madrid | 3 | (0) |
1997–1998 | → Leganés (mkopo) | 30 | (4) |
1999 | → Espanyol (mkopo) | 0 | (0) |
2000 | → Mallorca (mkopo) | 19 | (6) |
2000–2004 | Mallorca | 120 | (48) |
2004–2009 | Barcelona | 145 | (108) |
2009–2011 | Internazionale | 67 | (33) |
2011– | Anzhi Makhachkala | 43 | (21) |
SPAIN BADO NAMBA MOJA UBORA DUNIANI - FIFA
Mabingwa wa Dunia timu ya taifa ya Spain bado ndio inaendelea kushika namba moja katika Listi ya viwango vya FIFA vya Ubora Duniani iliyotolewa leo ikifuatiwa na timu ya taifa ya ujerumani ambapo nafasi ya tatu inashikiliwa na Argentina ambapo nafasi ya nne ikishikiliwa na Croatia, huku Tanzania Taifa star ikipanda Nafasi 7 kutoka 116 hadi 109.
Katika 10 Bora, Netherlands imepanda mpaka Nafasi ya 5, Portugal kushuka Nafasi moja hadi ya 6, Colombia, wameshuka Nafasi 2 na wapo nafasi ya 7 huku timu ya taifa ya England ikiporomoka Nafasi 2 na sasa wako Nafasi ya 9.
Kwa Nchi za Afrika, Côte d'Ivoire ndio ipo Nafasi ya juu kabisa ikiwa Nafasi ya 13 ikifuatiwa na Ghana iliyokatika Nafasi ya 20.
Brazil, ambayo imeathirika kwa kucheza Mechi za Kirafiki tu kwa Miaka miwili, imeporomoka Nafasi 2 hadi Nafasi ya 22 lakini kushiriki kwao katika Mashindano rasmi ya FIFA ya kugombea Kombe la Mabara yatakayochezwa Nchini brazil kuanzia Juni 15 kama watafanya vizuri basi itawaletea faida nzuri na sana katika harakati za kupanda chati.
Toleo jingine la Listi ya FIFA ya Ubora Duniani litatolewa Julai 4.
25 BORA:
1 Spain
2 Germany
3 Argentina
4 Croatia
5 Netherlands
6 Portugal
7 Colombia
8 Italy
9 England
10 Ecuador
11 Russia
12 Belgium
13 Côte d'Ivoire
14 Switzerland
15 Bosnia-Herzegovina
16 Greece
17 Mexico
18 France
19 Uruguay
20 Denmark
21 Ghana
22 Brazil
23 Mali
24 Czech Republic
25 Chile
NCHI ZINAZOIZUNGUKA TANZANIA:
104 Qatar
105 Lithuania
106 Ethiopia
107 Niger
108 Saudi Arabia
109 Malawi
109 Tanzania {imepanda nafasi 7]
111 Kuwait
112 Tajikistan
113 Suriname
114 Korea DPR
115 Benin 308
116 Northern Ireland
JESUS AONGEZEWA MKATABA MPYA NDANI YA KLABU YA BENFICA.
KLABU ya Benfica ya Ureno imetangaza kumuongezea mkataba mpya kocha wake Jorge Jesus atakao dumu nao klubuni hapo mpaka katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka 2015. Kulikuwa na wasiwasi kama kocha huyo mwenye umri wa miaka 58 anaweza kubakia katika klabu hiyo baada ya kumaliza msimu na kuambulia patupu. Hata hivyo Jesus sasa amemaliza utata huo kwa kusaini miaka miwili zaidi na klabu hiyo inayotoka katika jijini Lisbon. Jesus alianza kuinoa Benfica kuanzia mwaka 2009 na kuingoza kushinda taji moja la Ligi Kuu na matatu ya Kombe la Ligi la nchi hiyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)