Friday, June 7, 2013

GAZIDIS ATHIBITISHA KUWA ARSENAL WENGER ATAONGEZA MKATABA MPYA.

MTENDAJI Mkuu wa The Gunners club ya Arsanal Ivan Gazidis ametanabaisha kuwa kocha wa timu hiyo Arsene Wenger anataka aongeze Mkataba wake mwishoni mwa msimu ujao na kuiongoza klabu hiyo kufanya vizuri katika soka ya Ulaya.
Mkataba wa Wenger unaisha mwakani na tayari amepata ofa kibao kuanzia nyumbani kwao Ufaransa, ambako Paris Saint-Germain na klabu yake ya zamani, Monaco zinamtaka.
Sign him up! Gazidis wants the French boss to extend his deal with Arsenal beyond next summer
Gazidis (chini kushoto) anataka Mfaransa aongeze Mkataba mwishoni mwa msimu ujao
Sign him up! Gazidis wants the French boss to extend his deal with Arsenal beyond next summer
Matokeo mabaya ya miaka ya karibuni yalitarajiwa kumuweka katika wakati mgumu kocha huyo mwenye umri wa miaka 63, lakini Gazidis anatarajia atabaki na kuunda kikosi cha nguvu.
Pato la mwaka la Arsenal linatarajiwa kuongezeka kwa Pauni Milioni 70, na kuwasogeza kwa wanaopata Pauni Milioni 300, Real Madrid, Barcelona, Manchester United na mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich.
Hiyo itawapa fursa ya kushindana na klabu hizo kununua wachezaji wa kuanzia Pauni Milioni 25 na kutaka mishahara ya kuanzia Pauni 200,000 kwa wiki kama Wayne Rooney, mmoja kati ya wachezaji inayowataka hivi sasa.
Klabu tatu za juu katika msimamo wa Ligi Kuu ya England, Manchester United, City na Chelsea zote zimebadilisha makocha wao, lakini Arsenal bado na imani na Wenger.

JOSE MOURINHO AJA NA KASI MPYA NA NGUVU MPYA KATIKA USAJILI".

Baada ya kukabidhiwa bikoba kwa mara ya pili ndani ya Chelsea jose mourinho amekuja kasi mapya ya kutafuta  washambuliaji kikosini hapo baada ya jana usiku kuanza mazungumzo na mchezaji mwenye thamani ya Pauni Milioni 50, Edinson Cavani wa Napoli, saa kadhaa baada ya kutoa ofa ya Pauni ya Milioni 34.9 kumnasa mshambuliaji wa Zenit St Petersburg, Hulk.
Kocha Mourinho ameorodhesha wachezaji wanne anaowataka wakiwemo kutoka Fiorentina, Stevan Jovetic na Manchester City, Edin Dzeko katika orodha hiyo.
Interest: Napoli have opened talks with Chelsea over Uruguay striker Edinson Cavani (left)
Napoli imeanza mazungumzo na Chelsea kuhusu mshambuliaji wa Uruguay, Edinson Cavani (kushoto)
Mourinho ameweka wzi na kuamini kuwa atamsajili mchezaji wa Pauni Milioni 25, Jovetic na kuwapiku Juventus, lakini anakabiliwa na ushindani kutoka klabu yake ya zamani, Real Madrid katika kuwania saini ya Cavani wakati Dzeko anaonekana kuwa mboni mbadala. Napoli haijakataa mpango wa kubadilishana Cavani na Dzeko na Manchester City, lakini mpango unaonekana kusinzia.
Rais wa Napoli, Aurelio de Laurentiis alisema jana usiku: "Kuna dhamira kutoka Chelsea kwa Cavani, watanipigia mimi saa chache zijazo. Nitafurahi akibaki, lakini ikiwa ataondoka atampata mbadala wake,".
Mshambuliaji wa Brazil, Hulk pia amethibitisha Mourinho anamtaka Stamford Bridge.
Target: Chelsea have made a £35m offer for Zenit St Petersburg's Brazilian forward Hulk
Chelsea imetoa ofa ya Pauni Milioni 35 kwa Zenit St Petersburg juu ya Mbrazil, Hulk.

MAN CITY YATANGAZA RASMI KUMTWAA KIUNGO WA KIBRAZILI FERNADINHO.

Mabingwa wa ligi kuu nchini uingereza msimu wa 2011-2012 klabu ya Manchester City imetangaza rasmi kumsajili kiungo wa kimataifa wa Brazil Fernadinho kutoka klabu ya Shakhtar Donetski ya Ukraine. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28 amekuwa katika rada za City kwa karibu msimu mzima na anajulikana nchini Uingereza kwa kuifungia klabu yake bao katika ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Chelsea katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi msimu uliopita. City ambao mpaka sasa hawajapa mbadala wa kocha Roberto Mancini aliyeondoka, hawakutoa taarifa zozote za kiasi cha fedha walizomnunulia mchezaji huyo lakini kumekuwa na tetesi katika vyombo vya habari nchini Uingereza kuwa amewagharimu kiasi cha paundi milioni 30. Akihojiwa Fernadinho amesema kuwa hayo ni mabadiliko, changamoto na nafasi aliyokuwa akiisubiria kwa kipindi kirefu na kuichezea City ni kama ndoto zake zimekuwa kweli. 

FALCAO AWEKA WAZI KUWA NIA KUBWA NI KUIPA MAFANIKIO MONACO.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Colombia, Radamel Falcao amesema nia yake kubwa ni kuisadia klabu ya Monaco ya Ufaransa kuwa moja ya klabu bora barani Ulaya kwa mara nyingine tena. Akihojiwa baada ya mazoezi na timu yake ya taifa jana Alhamisi Falcao amesema anajisikia fahari kubwa kuwapo Monaco hivyo kutokana na kuvutiwa na mipango waliyokuwa nayo katika kipindi kijacho hivyo mategemeo yao nikuifikisha timu hiyo katika anga za mafanikio. Akiwa Monaco nyota huyo wa zamani wa klabu ya Atletico Madrid ataungana na winga James Rodriguez ambaye pia ni raia wa Colombia baada ya kukubali uhamisho akitokea klabu ya FC Porto. Falcao amesema ana mahusiano mazuri na winga huyo na sio katika soka pekee bali wamekuwa marafiki wa karibu hata nje ya uwanja, na kummwagia sifa kwamba ni mchezaji bora ndio maana Monaco wametumia fedha nyingi kumsajili. 

BOLT MKALI WA MBIO FUPI DUNIANI KUKABIDHI ZAWADI NCHINI UFARANSA.

SHIRIKISHO la Tenisi nchini Ufaransa limetangza kuwa mshindi wa michuano ya wazi ya Ufaransa kwa upande wa wanaume atakabidhiwa zawadi na mkimbiaji nyota wa mbio fupi duniani raia wa Jamaica Usain Bolt.

Bolt bingwa mara sita wa michuano ya Olimpiki ambaye jana alishindwa kutamba katika mashindano ya Diamond League yaliyofanyika jijini Rome itali baada ya kushindwa na Justin Gatlin wa Marekani, atakuwa mwanariadha wa kwanza kupata heshima hiyo kwenye michuano mikubwa ya tenisi. 

Nusu fainali kwa upande wanaume inatarajiwa kufanyika leo ambapo bingwa mtetezi wa michuano hiyo Rafael Nadal anatarajia kuchuana na Novak Djokovic ukifuatiwa na mchezo mwingine wa nusu fainali kati ya Jo-Wilfried Tsonga dhidi ya David Ferrer. Kwa upande wa wanawake ambapo fainali itafanyika Jumamosi kati ya Serena Williams na maria Sharapova, tuzo yao itakabidhiwa na bingwa mara tatu wa zamani wa michuano hiyo ambaye pia amewahi kuongoza katika orodha za ubora kwa wanawake Arantxa Sanchez Vicario wa Hispania. 

Thursday, June 6, 2013

GALLIANI ASEMA HATUNA MPANDO NA KAKA KUJA MILAN.

Adriano Galliani ambaye ni ofisa mkuu wa klabu ya AC Milan ya Italia,ametanabaisha na kuweka wazi kuwa klabu hiyo haina mpango wa kumsajili kiungo wa klabu ya Real Madrid Kaka ambapo amesema mchezaji huyo ameshakuwa mtu mzima. Kaka mwenye umri wa miaka 31 amekuwa akihusishwa na tetesi za kurejea San Siro kwa zaidi ya mara moja toka alipoondoka Milan kwenda Madrid mwaka 2009 lakini Galliani amekanusha tetesi hizo za kumsajili nyota huyo kutokana na umri wake. Kiungo huyo mshambuliaji bado ana mkataba na Madrid naomalizika katika kipindi majira ya kiangazi mwaka 2015 lakini anategemewa kuondoka katika klabu hiyo kutokana na kushindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza kwa miaka kadhaa sasa. Kaka amecheza mechi 19 pekee katika msimu wa 2012-2013 na kufunga mabao matatu. 

ETO"O ATWAA MCHEZAJI BORA WA LIGI NCHINI URUSI.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Cameroon na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi Samuel Eto’o ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa msimu wa Ligi Kuu ya nchi hiyo kwa msimu wa 2012-2013. Eto’o ambaye amewahi kunyakuwa tuzo ya mchezaji bora Afrika mara nne, alikabidhiwa tuzo hiyo baada ya kuisadia timu yake kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wan chi hiyo. Akihojiwa mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo Eto’o ambaye pia ni nahodha wa timu hiyo amedai kufurahishwa na hatua hiyo na kuwashukuru mashabiki wa soka nchini humo pamoja na waandishi wa habari kwa kuwa nyuma yake wakati wote. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 atakosa mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 wa timu ya taifa ya nchi yake dhidi ya Togo utakaochezwa Juni 9 mwaka huu kutokana na majeraha yanayomsumbua. 
SAMWELI ETO'O KATIKA ULIMWENGU WA SOKA
Samuel 2011.jpg
Eto'o in 2011.
Kuhusu yeye
Full nameSamuel Eto'o Fils
Date of birth10 March 1981 (age 32)
Place of birthDoualaCameroon[1]
Height1.80 m (5 ft 11 in)[2]
Playing positionStriker
Timu
Current clubAnzhi Makhachkala
Number9
academy
1992–1997Kadji Sports Academy
Timu za ukubwa
YearsTeammechi(Goli)"
1997–2000Real Madrid3(0)
1997–1998→ Leganés (mkopo)30(4)
1999→ Espanyol (mkopo)0(0)
2000→ Mallorca (mkopo)19(6)
2000–2004Mallorca120(48)
2004–2009Barcelona145(108)
2009–2011Internazionale67(33)
2011–Anzhi Makhachkala43(21)