Thursday, June 13, 2013

LIONEL MESSI NA MZAZI WAKE WA KIUME WAINGIA MATATANI.

Mshambuliaji nyota  wa Barcelona  na timu ya Taifa ya Argentina Lionel Messi na babake wanatuhumun kwa tuhuma za kukwepa kulipa kodi nchini Hispania huivyo serikali ya nchi hiyo ipo katika zaidi ambapo inasadikika kuwa na deni la paundi milioni tatu nukta nne.

Mchezaji huyo kutoka Argentina na babake, Jorge wanatuhumiwa kuibia serikali ya nchi hiyo, kwa kujaza fomu zisizokuwa za ukweli za marejesho ya kodi kati ya mwaka wa 2007 na 2009.Hata hivyo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hajasema lolote kuhusiana na madai hayo.
Messi hulipwa Euro milioni kumi na sita kila mwaka na ndiye mchezaji anayelipwa kiasi cha juu zaidi duniani.Lakini mwendesha mashtaka Raquel Amado, aliwasilisha nyaraka za mahakama nyumbani kwa mchezaji huyo katika mtaa wa kifahari wa Gava mjini Barcelona.
Jaji mjini humo ni sharti waidhinisha malalamishi dhidi ya mshukiwa yeyote kabla hajafunguliwa mashtaka.Messi na babake wanashukiwa kutumia kampuni katika mataifa ya ng’ambo, mjini Belize na Uruguay kuuza haki za kutumia picha ya mchezaji huyo.
Mchezaji huyo na babake wanatuhumiwa kutumia kampuni hizo zilizoko nje ya Hispania, ambako anaishi na kucheza soka ya kulipwa, kukwepa kulipa kodi inayokisiwa kuwa paundi milioni tatu na nusu.

MASCHERANO AOMBA RADHI KUMPIGA TEKE DAKTARI WA TIMU:

KIUNGO nyota wa Club ya Barcelona na timu ya  taifa ya Argentina Javier Mascherano ameomba radhi baada ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kosa la kumpiga teke daktari wakati wa mechi ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kati ya timu ya taifa ya nchi yake na Ecuador.
Kiungo huyo ambaye kucheza katika vilabu vya Liverpool na West Ham United alitolewa baada ya kumpiga teke dereva wa gari maalumu la kubebea wachezaji walioumia dakika ya 87 ya mchezo huo. 
Nyota huyo ambayo alikuwa nahodha katika mchezo huo aliomba radhi kwa tukio hilo na kudai kuwa alimuonya dereva kwa kwenda kasi mpaka kutaka kumdondosha ingawa amedai alichokifanya hakikubaliki.
Katika mchezo huo Argentina ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi Ecuador na kuendelea kubakia kileleni wakiwa na alama 27 wakifuatiwa na Colombia waliopo nafasi ya pili wakiwa na alama 26 huku Ecuador wakibakia nafasi ya tatu wakiwa na alama 22.

ESSIEN ASEMA NIPOM TAYARI KUCHEZA NAFASI YOYOTE UWANJANI:

KIUNGO nyota wa Chelsea na timu ya Taifa ya Ghana Michael Essien amesema kuwa amejiandaa kucheza nafasi yoyote chini ya kocha mpya wa klabu hiyo Jose Mourinho. Kiungo huyo wa kimataifa wa Ghana alikuwa akipewa nafasi kidogo ya kucheza chini Roberto Di Matteo baada kusumbuliwa na majeraha ya mguu lakini alipata ahueni wakati Mourinho alipomwita kwa mkopo wakati akifundisha Real Madrid. Mourinho amekuwa akimchezesha Essien kama beki au kiungo wakati akiwa Santiago Bernabeu na sasa yuko tayari kucheza nafasi yoyote ambayo Mreno huyo atamchezesha. Essien mwenye umri wamiaka 30 alisajiliwa na Mourinho wakati akiwa Chelsea mwaka 2005 kwa ada ya paundi milioni 29 akitokea klabu ya Lyon ya Ufaransa.

Wednesday, June 12, 2013

MWAIKIMBA KATIKA HARAKATI ZA MAISHA YA SOKA:

JINA KAMILI: Gaudence Mwaikimba
KUZALIWA: Oktoba 5, 1984

ALIPOZALIWA: Kyela, Mbeya 
KLABU YAKE: Azam FC

NAFASI UWANJANI; Mshambuliaji

UREFU; 189 cm

UZITO; 85 kg

KLABU ZA AWALI:

MWAKA              CLUB 

2003-2004:        Tukuyu Stars

2004- 2005:       Kahama United

2005- 2006:       Ashanti United

2006- 2009:       Yanga SC 
2009-2010:        Sur (Oman)

2010:                 Prisons FC

2011- 2012:        Kagera Sugar

2012:                  Moro United

2012 hadi sasa     Azam FC 

WASIFU 
Baadhi ya Picha Zikimuonyesha Gaudence Mwaikimba akiwa n

DAVID VILLA KATIKA ULIMWENGU WA SOKA JE WAMJUA?

David Villa
David Villa2 (cropped).jpg
Villa in 2008
Personal information
Full nameDavid Villa Sánchez[]
Date of birth3 December 1981 (age 31)]
Place of birthLangreo, Spain
Height1.75 m (5 ft 9 in)[2]
Playing positionStriker
Club information
Current clubBarcelona
Number7
Youth career
1991–1999Langreo
Senior career*
YearsTeamApps(Gls)
1999–2001Sporting Gijón B65(25)
2001–2003Sporting Gijón80(38)
2003–2005Zaragoza73(32)
2005–2010Valencia166(108)
2010–Barcelona77(33)
National team
2000–2003Spain U217(0)
2005–Spain88(53)
2002Asturias1(0)

CLUB MATAJI

Real Zaragoza
Valencia
Barcelona


SIMBA NA YANGA YAZIWEKEA NGUMU KUSHIRIKI MICHUANO YA KAGAME-SERIKALI


SERIKALI imesisitiza kuwa timu za Simba na Yanga hazitashiriki katika michuano ya klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati maarufu kama kombe la Kagame. Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Amos Makala ametoa taarifa hiyo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Sumve Mheshimiwa Richard Ndasa. Katika swali lake mheshimiwa Ndasa ametaka kujua msimamo wa Serikali juu ya timu za Simba na Yanga kushiriki michuano ya Kagame inayotarajia kuanza Juni 18 hadi Julai 2, mwaka huu huko Sudan Kusini. Akijibu swali hilo mheshimiwa MAKALA amesema kumekuwa na taarifa za hali ya usalama katika Nchi ya Sudan kuwa sio nzuri. Amesema kumekuwa na taarifa kulingana na hali ya usalama nchini Sudan na kwamba Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mheshimiwa Benard Membe tayari amelitolea taarifa na ndani ya Serikali kuna taarifa za kutosha kuwa Sudan hakuna usalama. Amesema msimamo wa Serikali ni kuwa hawawezi kupeleka timu mahali ambapo hakuna usalama.

KIKOSI CHA IVORY COAST KUWASILI JUNI 13


Msafara wa timu ya Taifa ya Ivory Coast (The Elephants) wa watu 80 wakiwemo wachezaji 27 unatarajiwa kuwasili nchini kesho (Juni 13 mwaka huu) kwa ndege maalum kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars.

Mechi hiyo itachezwa Jumapili (Juni 16 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri, na itachezeshwa na Charef Mehdi Abdi kutoka Algeria.

Kikosi hicho kitawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 2.50 usiku na kitafikia hoteli ya Bahari Beach iliyoko nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Timu hiyo inatarajia kuondoka saa chache baada ya mechi hiyo.

Wachezaji walioko katika kikosi hicho ni Abdoul Razak, Akpa Akpro Jean-Daniel Dave Lewis, Angoua Brou Benjamin, Arouna Kone, Aurier Serge Alain Stephane, Bamba Souleman, Barry Boubacar, Boka Etienne Arthur, Bolly Mathis Gazoa Kippersund, Bony Wilfried Guemiand, Cisse Abdoul Karim, Diarrassou Ousmane Viera na Dja Djedje Brice Florentin.

Doumbia Seydou, Gbohouo Guelassiognon Sylvain, Gosso Gosso Jean-Jacques, Kalou Salomon Armand Magloire, N’dri Koffi Christian Romaric, Sangare Badra, Serey Die Gnonzaroua Geoffroy, Sio Giovanni, Tiote Cheik Ismael, Toure Yaya Gnegneri, Traore Lacina, Ya Konan Didier, Yao Kouassi Gervais na Zokora Deguy Alain Didier.

Taifa Stars iko kambini hoteli ya Tansoma tangu iliporejea kutoka Marrakesh, Morocco ambapo leo na kesho itafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri. Ijumaa itapumzika, na itafanya mazoezi ya mwisho Jumamosi kwenye uwanja huo huo kuanzia saa 10 kamili.

Makocha wa timu zote mbili (Taifa Stars na The Elephants) watakutana na waandishi wa habari Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF kuzungumzia jinsi walivyojiandaa kwa mechi hiyo.

KIINGILIO MECHI YA STARS, IVORY COAST 5,000/-
Kiingilio cha chini katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Ivory Coast (The Elephants) itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani.

Viti vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kumeza watazamaji 60,000 viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 ni sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 ni sh. 10,000.

Viingilio vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.

Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza kuuzwa siku mbili kabla ya mchezo (Ijumaa na Jumamosi) katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.

Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi. Tunapenda kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.

Utaratibu katika mechi hiyo utakuwa kama ilivyokuwa katika mchezo wa Simba na Yanga, ambapo hayataruhusiwa kuingia uwanjani isipokuwa kwa yale yatakayokuwa na sticker maalumu kutoka TFF.

HATUA YA TATU RCL KUCHEZWA JUMAMOSI
Mechi za kwanza za hatua ya tatu ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao zitachezwa Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) wakati za marudiano zitachezwa Jumatano ya Juni 19 mwaka huu.


Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana jana (Juni 11 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za michezo iliyopita na kufanya uamuzi mbalimbali ikiwemo mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars na Machava FC ambayo haikuchezwa.

Machava FC ambayo ilishinda mechi ya kwanza iliyochezwa mjini Moshi kwa mabao 2-0 inaendelea katika hatua ya tatu kwa vile haikuhusika katika kukwamisha mchezo wa marudiano uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kiliuhamishia mchezo huo kwenye Uwanja wa Mgambo mjini Mpwapwa kinyume na maelekezo ya Kamati ya Mashindano ya TFF. Kamati katika kikao chake cha awali iliekeleza kuwa mechi zote za RCL zitachezwa makao makuu ya mikoa isipokuwa kwa Morogoro ambapo timu ya Techfort FC iliruhusiwa kutumia Uwanja wa CCM Mkamba mjini Ifakara.

Hivyo timu nane zilizofuzu kucheza raundi hiyo ni Friends Rangers ya Dar es Salaam, Kariakoo ya Lindi, Katavi Warriors ya Katavi, Kimondo SC ya Mbeya, Machava ya Kilimanjaro, Njombe Mji ya Njombe, Polisi Jamii ya Mara na Stand United FC ya Shinyanga.

Wakati timu nyingine zimefuzu kwa kushinda mechi zao za raundi ya mbili, Njombe Mji imeingia hatua hiyo kwa kuwa timu yenye uwiano mdogo wa kufungwa (best looser) katika hatua ya pili.

Katika hatua hiyo mechi ni ifuatavyo; Kariakoo vs Friends Rangers, Machava FC vs Stand United FC, Polisi Jamii vs Katavi Warriors, na Kimondo SC vs Njombe Mji. Timu zilizoanza kutajwa ndizo zinazoanzia nyumbani.

Vilevile Kamati ya Mashindano imeagiza Kamishna wa mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars vs Machava FC, Mwijage Rugakingira wa Tanga ambaye alikwenda Uwanja wa Mgambo badala ya Uwanja wa Jamhuri kinyume na maelekezo ya TFF aondolewe kwenye orodha ya makamishna.

Pia waamuzi wa mechi hiyo ambao nao walikwenda Mpwapwa badala ya Dodoma Mjini wamepelekwa Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya kuchukuliwa hatua kutokana na tukio hilo.

Kamati ya Mashindano imekumbusha kuwa RCL ni mashindano yanayosimamiwa na TFF, hivyo maelekezo yoyote kuhusiana na mashindano hayo pia yatatoka TFF na si mahali pengine popote. Hivyo, msimamizi wa kituoa hana mamlaka ya kubadili uwanja.

Hatua ya nne ya RCL itachezwa kati ya Juni 23 na 23 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 29 na 30 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)