TIMU
ya soka ya African Lyon ya jijini Dar es Salaam imetangaza hasara ya
sh. milioni 180.3 kutokana na ushiriki wake katika msimu uliopita wa
Ligi Kuu Tanzania Bara.
Lyon ni miongoni mwa timu tatu
zilizoshuka daraja kutoka katuika ligi hiyo kubwa ya soka nchini,
nyingine ni Toto African na Polisi Moro.
Salim
amesema katika makusanya na matumizi yao, walilazimika kutumia kiasi
cha sh. milioni 268.09 katika mzunguko wa kwanza, kabla ya kutumia sh.
123.6.
"Katika matumizi yote haya, fedha ambayo tumeiingiza kama
klabu kupitia viingilio na vyanzo vingine ni sh. milioni 207.6, na hapo
ndipo unapopata tofauti ya sh. milioni 180.3, ambayo ni hasara," Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Lyon, Rahim Kangezi,
alisema soka ya Tanzania inaendeshwa kwa hasara huku wenye dhamana ya
kusaidia wakiwa hawatendi haki kwa baadhi ya vipengele.
Kangezi alisema timu yake imeingia katika hasara ya sh. milioni 180.3 kutokana na uendeshaji, lakini bado wameshuka daraja, huku akisisitiza kuwa hakuna anayeshutumiwa kwa kushuka kwa timu hiyo"Unaweza kuona changamoto ambayo tunakumbana nayo katika uendeshaji wa taasisi kamam a hizi, tunapopiga kelele kwa wadhamini kutuwahishia fedha tunamaanisha."Angalieni mfano mdogo kwa fedha za wadhamini (Vodacom), ambazo awamu ya mwisho zimetufikia Mei mwaka huu, tukiwa tumebakiza mechi moja ya Ligi Kuu, sasa zingetusaidia katika nini? Alihoji mmiliki huyo.
Kangezi alisema timu yake imeingia katika hasara ya sh. milioni 180.3 kutokana na uendeshaji, lakini bado wameshuka daraja, huku akisisitiza kuwa hakuna anayeshutumiwa kwa kushuka kwa timu hiyo"Unaweza kuona changamoto ambayo tunakumbana nayo katika uendeshaji wa taasisi kamam a hizi, tunapopiga kelele kwa wadhamini kutuwahishia fedha tunamaanisha."Angalieni mfano mdogo kwa fedha za wadhamini (Vodacom), ambazo awamu ya mwisho zimetufikia Mei mwaka huu, tukiwa tumebakiza mechi moja ya Ligi Kuu, sasa zingetusaidia katika nini? Alihoji mmiliki huyo.
Akizungumzia
kuhusu uendeshwaji wa Ligi Kuu na changamoto walizokutana nazo, Kangezi
alisema bado hakujakuwa na usimamizi mzuri katika kuhakikisha kuwa ligi
hiyo inakuwa bora.
"Tulifanikiwa pia kuileta timu kubwa ya Ligi
Kuu ya Brazil (Atletico Parenese) kwa ziara ya kimichezo nchini, tulitoa
wachezaji watano kwa ajili ya kujaribu soka ya kulipwa sambamba na
kufanya semina mbili juu ya uongozi wa michezo," aliongeza.