Wednesday, February 12, 2014

WAZIRI UMMY MWALIMU AFUNGUA MAFUNZO YA SIKU MBILI KWA MADIWANI WANAWAKE KUTOKA HALMASHAURI ZA MKOA WA TANGA

NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS,UMMY MWALIMU AKIUZNGUMZA WAKATI WA WARSHA YA MAFUNZO KWA MADIWANI WOTE WANAWAKE KUTOKA HALMASHAURI ZOTE MKOANI TANGA.
BAADHI WA WASHEMIWA MADIWANI KUTOKA HALMASHAURI MBALIMBALI MKOANI TANGA WAKIFUATILIA MADA MBALIMBALI KWENYE WARSHA YA MAFUNZO KWA MADIWANI WANAWAKE .










MJUMBE WA BODI YA  TAWODE NA MWENYEKITI WA JUMUIYA WA UMOJA WA VIJANA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA TANGA (UVCCM),ABDI MAKANGE AKIZUNGUMZA KWENYE MAFUNZO HAYO LEO
MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO KULIA AKIWA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA TAWODE FATUMA MGANGA KUSHOTO KWENYE MAFUNZO HAYO LEO
NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS UMMY MWALIMU KATIKATI KUSHOTO NI MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO NA KULIA NI KATIBU WA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA TANGA,GUSTAV MUBBA WAKIWA KWENYE WARSHA YA MAFUNZO YA SIKU MBILI KWA MADIWANI WOTE MKOA WA TANGA.  
HAPA WAKIPIGA MAKOFI.
NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS UMMY MWALIMU KATIKATI KUSHOTO NI MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO  NA KULIA NI KATIBU WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) MKOA WA TANGA,GUSTAV MUBBA LEO WAKATI WA MAFUNZO YA SIKU MBILI KWA MADIWANI WANAWAKE KUTOKA HALMASHAURI ZOTE ZA JIJI LA TANGA

Sunday, February 9, 2014

SERIE A: JUVE YALAZIMISHWA SARE YA BAO 2-2 VS VERONA-TEVEZ ATUPIA

MBALI ya Juventus kutangulia kwa Bao 2 za mapema kupitia Carlos Tevez, Hellas Verona walijipanga na hatimaye kurudisha Bao zote na kupata Sare ya Bao 2-2 walipocheza na Mabingwa hao wa Italy ambao pia ni Vinara wa Serie A huko Italy.

Baada Tevez kupiga Bao 2, Luca Toni aliifungia Hellas Verona Bao la kwanza na Muargetina Juanito Gomez kusawazisha katika Dakika ya 94.

Baada ya hii Leo Timu ya Pili AS Roma nao kubanwa na kutoka Sare 0-0 Lazio, Juve wamebaki kileleni wakiwa Pointi 9 mbele ya AS Roma na wako Pointi 13 mbele ya Timu ya Tatu Napoli ambao waliifunga AC Milan 3-1 hapo Jana Jumamosi.

RATIBA/MATOKEO:

Jumapili Februari 9

Torino 1 Bologna 2

Lazio 0 AS Roma 0

Parma 0 Catana 0

Sampdoria 1 Cagliari 0

Livorno 0 Genoa 1

Hellas Verona 2 Juventus 2

2245 Inter Milan v Calcioa

MSIMAMO-Timu za Juu:

NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Juventus FC 23 19 3 1 56 18 38 60
2 AS Roma 22 15 6 1 45 11 34 51
3 SSC Napoli 23 14 5 4 47 27 20 47
4 Fiorentina 23 13 5 5 42 24 18 44
5 Hellas Verona 23 11 3 9 39 37 2 36
6 Inter Milan 22 8 9 5 39 27 12 33

TFF YATANGAZA BODI YA WADHAMINI NA KAMATI ZAKE!!

BOARD OF TRUSTEE; Said Hamad El-Maamry, Stephen Mashishanga, Dr Ramadhan Dau, Joel Bendera, Mohamed Abdul Aziz

Kamati ya Nidhamu; Tarimba Abbas (Mwenyekiti), Advocate Jerome Msemwa (Makamu Mwenyekiti), Kassim Dau, Nassoro Duduma, Kitwana Manara.
Kamati ya Rufani ya Nidhamu; Profesa Mgongo Fimbo (Mwenyekiti), Advocate Hamidu Mbwezeleni (Makamu Mwenyekiti), Titus Bandawe, Twaha Mtengera, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) mstaafu Boniface Mpaze.
Kamati ya Maadili; William Erio (Mwenyekiti), Advocate Ezekiel Maganja (Makamu Mwenyekiti), Advocate Victoria Mandari, Kanali mstaafu Enos Mfuru na Said Mtanda.
Kamati ya Rufani ya Maadili; Jaji mstaafu Stephen Ihema (Mwenyekiti), Wakili Alesia Mbuya (Makamu Mwenyekiti), Lilian Kitomari, Jabir Shekimweri na Chabanga Hassan Dyamwale.
Kamati ya Uchaguzi; Advocate Melchesedeck Lutema (Mwenyekiti), Advocate Walter Chipeta (Makamu Mwenyekiti), Hamidu Mahmoud Omar, Jeremiah John Wambura, Hassan Dalali.
Kamati ya Rufani ya Uchaguzi; Advocate Julius Lugaziya (Mwenyekiti), Advocate Mwita Waissaka (Makamu Mwenyekiti), Juma Abeid Khamis, Rashid Dilunga, Masoud Issangu.
Kamati ya Fedha na Mipango; Wallace Karia (Mwenyekiti), Francis Ndulane (Makamu Mwenyekiti), Omari Walii, Eliud Mvella, Said Muhammad, Geofrey Nyange, Kidao Wilfred, Ayoub Nyenzi, Lina Kessy, Cyprian Kuhyava.
Kamati ya Mashindano; Geofrey Nyange (Mwenyekiti), Clement Sanga (Makamu Mwenyekiti), Msafiri Mgoyi, James Mhagama, Mohamed Nassoro, Moses Katabaro, Seif Ahmed, Gerald Ambi, Davis Mosha, Said George, Nassoro Idrissa (Mshauri wa Rais Ufundi- Pelegrinius Rutayuga).
Kamati ya Ufundi; Kidao Wilfred (Mwenyekiti), Athumani Kambi (Makamu Mwenyekiti), Vedastus Lufano, Blassy Kiondo, Rahim Kangezi, Patrick Kahemele, Daud Yassin, Nicholas Mihayo, Dk. Cyprian Maro (Mshauri wa Rais Ufundi- Pelegrinius Rutayuga).
Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana; Ayoub Nyenzi (Mwenyekiti), Khalid Abdallah (Makamu Mwenyekiti), Ali Mayay, Mulamu Ng’hambi, Apollo Kayungi, Said Tully, Luteni Kanali Charles Mbuge, Lameck Nyambaya, Ibrahim Masoud (Mshauri wa Ufundi wa Rais- Pelegrinius Rutayuga).
Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake; Lina Kessy (Mwenyekiti), Shyrose Bhanji (Makamu Mwenyekiti), Zena Chande, Amina Karuma, Dk. Cecilia Makafu, Zafarani Damoder, Beatrice Mgaya, Sofia Tigalyoma, Martin Mung’ong’o, Ingridy Kimaro.
Kamati ya Waamuzi; Saloum Umande Chama (Mwenyekiti), Nassoro Said (Makamu Mwenyekiti), Charles Ndagala (Katibu), Riziki Majala, Kanali Isaro Chacha, Paschal Chiganga, Victor Mwandike, Soud Abdi, Zahra Mohamed.
Kamati ya Habari na Masoko; Hamad Yahya Juma (Mwenyekiti), Naibu Waziri January Makamba (Makamu Mwenyekiti), Tido Mhando, Yusuf Manji, Yusuf Bakhresa, Samwel Nyalla, Jack Gotham, Fredrick Mwakalebela, Juma Pinto.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji; Advocate Richard Sinamtwa (Mwenyekiti), Advocate Moses Kaluwa (Makamu Mwenyekiti), Zacharia Hans Poppe, Hussein Mwamba, Philemon Ntahilaja, Abdul Sauko, Imani Madega.
Kamati ya Ukaguzi wa Fedha; Ramadhan Nassib (Mwenyekiti), Zitto Kabwe (Makamu Mwenyekiti), Nicholas Magarinza, Jackson Songora, Epaphra Swai, Kalilo Samson, Goodluck Moshi, Golden Sanga, Elias Mwanjala.
Kamati ya Tiba; Dk. Paul Marealle (Mwenyekiti), Dk. Fred Limbanga (Makamu Mwenyekiti), Dk. Mwanandi Mwankemwa, Dk. Nassoro Matuzya, Dk. Eliezer Ndelema, Asha Sadick.
Kamati ya Mpira wa Miguu wa Ufukweni; Ahmed Idd Mgoyi (Mwenyekiti), Shaffih Kajuna Dauda (Makamu Mwenyekiti), Boniface Pawasa, Deo Lucas, Juma Mgunda, John Kanakamfumu, John Mwansasu.
AD HOC COMMITTEES
Kamati ya Kutathimini Muundo wa Ligi; Dk. Mshindo Msolla (Mwenyekiti),Idd Mshangama (Katibu), Rahim Kangezi, Amri Said, Sunday Manara, Salim Bawazir, Lucas Kisasa.
Kamati ya Kutathimini Muundo wa Bodi ya Ligi; David Nchimbi (Mwenyekiti), Edwin Kidifu, Jones Paul, Evans Aveva, John Jambele, Masoud Sanani, Pelegrinius Rutayuga.

SIMBA YABAMIZWA NA WAZEE WA KWATA JKT MGAMBO

WEKUNDU wa Msimbazi Simba imelala bao 1-0 jioni ya leo mbele ya Mgambo Shooting Uwanja wa Mkwakwani, Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Kwa mara nyingine leo kipa Ivo Mapunda amefungwa bao rahisi, baada ya kumtemea mpira mshambuliaji Fully Maganga dakika ya 29 kufuatia mpira wa adhabu. Wachezaji wa Simba SC walipambana sana kujaribu kusawazisha bao hilo tangu hapo, lakini Mgambo Shooting leo walisimama imara kuhakikisha wanaondoka na pointi tatu.
Kwa matokeo hayo, Simba SC inabaki na pointi zake 31 baada ya kucheza mechi 17, wakati Mgambo inatimiza pointi 12 na inaendelea kushika mkia.
Kikosi cha Simba SC leo kilikuwa; Ivo Mapunda, Haruna Shamte/Ramadhani Chombo ‘Redondo’ dk57, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Amri Kiemba, Awadh Juma/Uhuru Suleiman dk62, Ramadhani Singano ‘Messi’, Amisi Tambwe na Ali Badru/Haroun Chanongo dk46.
Mgambo Shooting; Saleh Tendega, Bashir Chanache, Salim Kipaga, Bakari Mtama, Novaty Lufunga, Mohamed Samatta, Peter Mwalyanzi, Bolly Ajali, Fully Maganga Malima Busungu.

Thursday, February 6, 2014

KANEMBWA JKT NA WACHEZAJI WAO KUJITETEA KAMATI YA NIDHAMU!

TFF_LOGO12TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 6, 2014
Wachezaji tisa wa Kanembwa JKT pamoja na timu yao wanaolalamikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kumpiga mwamuzi Peter Mujaya wanatakiwa kujitetea mbele ya Kamati ya Nidhamu itakayokutana Jumapili (Februari 9 mwaka huu).
Utetezi huo unaweza kuwa wa mdomo kwa walalamikiwa kufika wenyewe mbele ya kamati itakayokutana saa 4 kamili asubuhi au kuuwasilisha kwa njia ya maandishi.
Kamati ilikutana jana Jumatano (Februari 5 mwaka huu) kusikiliza malalamiko dhidi ya wachezaji hao na timu yao kwa tukio hilo lililotokea Novemba 2 mwaka jana kwenye mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) dhidi ya Stand United FC iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Wachezaji hao ni Abdallah Mgonja, Bariki Abdul, Philipo Ndonde, Mbeke Mbeke, Mkuba Clement, Mrisho Mussa, Nteze Raymond, Ntilakigwa Hussein na Uhuru Mwambungu. Mlalamikiwa mwingine ambaye naye anatakiwa kujitetea ni timu ya Kanembwa JKT.
Ikiwa chini ya Mwenyekiti wake Tarimba Abbas, Kamati hiyo baada ya kusikiliza malalamiko dhidi ya wahusika na kupokea ushahidi wa aina mbalimbali kutoka kwa mlalamikaji imesema ili iweze kutenda haki katika shauri hilo ni lazima walalamikiwa wapate fursa ya kusikilizwa.
Katika hatua nyingine, Kamati hiyo iliyokutana kwa mara ya kwanza tangu ilipoundwa imesema imesikitishwa na vitendo vya fujo ndani ya mpira wa miguu, na kuwataka watu wasijihusishe na aina yoyote ya fujo.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Wednesday, February 5, 2014

LOGARUSIC AFUNGUKA KUHUSU MTIBWA

Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, ametanabaisha na kufunguka kuwa, anahofia kikosi chake kupata majeruhi katika kipindi hiki cha lala salama kwani watamharibia mipango yake.
 
Simba ipo nafasi ya nne ya msimamo wa ligi kuu kufuatia kuwa na pointi 30, nyuma ya Mbeya City yenye pointi 31, ambapo inahitaji kujipanga ili iweze kufanikiwa kusonga mbele.
Loga alisema anahofia majeruhi katika kikosi chake kwani wanaweza kusababisha kutokuwa na kikosi kizuri kwa kuwa kila mchezaji anamtumia kulingana na mfumo.
Ligi ni ngumu na hakuna timu kubwa wala ndogo katika kipindi hiki kwani kila timu imejiandaa vya kutosha, hivyo tunahitaji kujipanga pindi tunapokutana na timu yoyote.
Kwa sasa sina kikosi cha kwanza na ninatumia mchezaji kulingana na mechi kwani kuna baadhi wanajua mfumo huu na wengine wanajua mfumo mwingine, hivyo wote wapo sawa.
Wachezaji ambao ni majeruhi kwa sasa ni Said Nassoro ‘Chollo’ ambapo Donald Musoti alikuwa anasumbuliwa na malaria, pia kuna baadhi ya wachezaji wanacheza huku wakisumbuliwa na majeraha madogo-madogo.

PAWASA NA WENGINE WATEULIWA KUSAKA VIPAJI KWA AJILI YA TAIFA STAR

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeteua kikosi cha makocha 40 kutoka sshehemu mbalimbali, Tanzania Bara na Zanzibar ili kung’amua vipaji katika mpango wa kuboresha timu ya Taifa (Taifa Stars).
Makocha hao ambao watafanya kazi hiyo katika michuano maalumu ya mikoa wanatakiwa kuripoti katika ofisi za TFF siku ya Jumamosi (Februari 8 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwa ajili ya kupewa maelekezo zaidi.
Walioteuliwa ni Abdallah Hussein (Kilimanjaro), Abdul Mingange (Dar es Salaam), Ali Bushiri (Zanzibar), Ali Mayay (Dar es Salaam), Ally Mtumwa (Arusha), Ayoub Selemani (Zanzibar), Boniface Pawasa (Dar es Salaam), Dan Korosso (Mbeya), Dk. Mshindo Msolla (Dar es Salaam) na Edward Hiza (Morogoro).
Elly Mzozo (Dar es Salaam), Fred Minziro (Dar es Salaam), George Komba (Dodoma), Hafidh Badru (Zanzibar), Hamimu Mawazo (Mtwara), Idd Simba (Mwanza), Jabir Seleman (Zanzibar), John Tegete (Mwanza), Juma Mgunda (Tanga) na Kanali mstaafu Idd Kipingu (Dar es Salaam).
Kenny Mwaisabula (Dar es Salaam), Khalid Abeid (Dar es Salaam), Madaraka Bendera (Arusha), Madaraka Selemani (Dar es Salaam), Mbarouk Nyenga (Pwani), Mohamed Mwameja (Dar es Salaam), Musa Kissoki (Dar es Salaam), Nicholas Mihayo (Dar es Salaam), Patrick Rweyemamu (Dar es Salaam) na Peter Magomba (Singida).
Peter Mhina (Songea), Salvatory Edward (Dar es Salaam), Salum Mayanga (Morogoro), Sebastian Nkoma (Dar es Salaam), Sekilojo Chambua (Dar es Salaam), Shaban Ramadhan (Zanzibar), Steven Nemes (Dar es Salaam), Sunday Manara (Dar es Salaam), Tiborowa Jonas (Dar es Salaam), Yusuf Macho (Dar es Salaam), Zamoyoni Mogela (Dar es Salaam).