Friday, March 28, 2014

BPL:ARSENAL KUIKARIBISHA MAN CITY UWANJANI EMIRATES".

Kesho Jumamosi Ligi Kuu nchini uingereza inaingia tena kilingeni kwa michezo 7 kuanzia Mechi ya Saa Tisa na dakika 45 katika uwanja wa Old Trafford kati ya Manchester United na Aston Villa na kumalizika Usiku kwa Bigi Mechi Uwanjani Emirates kati ya Arsenal na Man City.
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumamosi Machi 29
15:45 Man United v Aston Villa
18:00 Crystal Palace v Chelsea
18:00 Southampton v Newcastle
18:00 Stoke v Hull
18:00 Swansea v Norwich
18:00 West Brom v Cardiff
20:30 Arsenal v Man Cit
Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, licha ya kukaririwa kukiri kwamba wao hawana nafasi ya kutwaa Ubingwa, ametamka kwamba bado lengo lao ni kuwa Mabingwa.
Amesema: “Hatuna kitu kingine zaidi ya kuwa Bingwa! Hiyo ndio azma yetu ya kwanza!”
Lakini Arsenal wanapambana na Man City ambayo iliwakung’uta Bao 6-3 Mwezi Desemba katika Mechi ya Ligi Uwanjani Etihad.
Wenger amesisitiza ni muhimu kwao kuonyesha nguvu Nyumbani kwao na hilo ndio litakalodhihirisha kama wana nafasi ya Ubingwa.
MSIMAMO:
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Chelsea 31 21 6 4 62 23 39 69
2 Liverpool 31 21 5 5 84 39 45 68
3 Man City 29 21 3 5 79 27 52 66
4 Arsenal 31 19 6 6 54 35 19 63
5 Everton 30 16 9 5 46 30 16 57
6 Tottenham 31 17 5 9 40 40 0 56
7 Man United 31 15 6 10 48 37 11 51
8 Newcastle 31 14 4 13 38 43 -5 46
9 Southampton 31 12 9 10 45 40 5 45
10 Stoke 31 9 10 12 36 45 -9 37
11 West Ham 31 9 7 15 34 41 -7 34
12 Aston Villa 30 9 7 14 33 42 -9 34
13 Hull 31 9 6 16 33 39 -6 33
14 Norwich 31 8 8 15 26 48 -22 32
15 Swansea 31 7 9 15 41 47 -6 30
16 West Brom 30 5 13 12 33 45 -12 28
17 Crystal Palace 30 8 4 18 19 39 -20 28
18 Sunderland 29 6 7 16 27 45 -19 25
19 Cardiff 31 6 7 18 26 58 -32 25
20 Fulham 31 7 3 21 30 70 -40 24
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumapili Machi 30
1530 Fulham v Everton
1800 Liverpool v Tottenham
Jumatatu Machi 31
2200 Sunderland v West Ham

Thursday, March 27, 2014

TFF YAANZA KUENDELEZA UWANJA WAKE MNYANJANI, TANGA

TFF YAANZA KUENDELEZA UWANJA WA TANGA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeanza mchakato wa kuendeleza uwanja wake uliopo eneo la Mnyanjani jijini Tanga.
TFF_LOGO12Shughuli inayoendelea kwa sasa ni kupima udongo (soil test) na kuandaa michoro kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha michezo (Sports Complex) ukiwemo uwanja wa mpira wa miguu na majukwaa yake.
TFF imetuma maombi rasmi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kuomba eneo la kujenga kituo cha michezo ikiwemo uwanja wa mipira wa miguu na majukwaa yake.
Pia Mkuu wa mkoa ameombwa kuingilia kati kuwaondoa wafanyabiashara waliovamia uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri (King George Memorial ground) mjini Moshi.
TFF YAANZA KUENDELEZA UWANJA WA TANGATFF inawakumbusha viongozi wa vyama vya mikoa ambao hawajaomba maeneo ya kujenga vituo vya michezo vikiwemo viwanja vya mpira wa miguu, waongeze jitihada za kufanya hivyo, TFF itawaunga mkono.
TFF inachukua fursa hii kuvipongeza vyama vya mpira wa miguu ambavyo ama tayari vimeshachukua hatua au viko mbioni kuchukua hatua kutafuta na kuendeleza maeneo kwa ajili ya matumizi ya mpira wa miguu.
TFF inaahidi kuunga mkono juhudi hizi na pale itakapohitajika kuongeza nguvu haitasita kufanya hivyo.
Wakati huo huo, TFF inalishukuru Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kwa kukubali kugharamia uwekaji nyasi za bandia kwenye Uwanja wa Kaitaba, na pia kusaidia uendelezaji wa uwanja wa TFF wa Tanga.
JAMAL MALINZI
RAIS
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

BPL-LIVERPOOL YAITUNGUA SUNDERLAND YAKWEA NAFASI YA PILI

Liverpool jana usiku imefanikiwa kuibuka na ushindi kwa Bao za Steven Gerrard na Daniel Stirridge zimewapa Liverpool ushindi wa Bao 2-1 walipocheza na Sunderland kwenye Mechi ya Ligi Kuu England na kuzidi kuwapa matumaini ya kuweza kutwaa Ubingwa Msimu huu.
Bao la Sunderland lilifungwa na Ki Su

WEST HAM 2 HULL CITY 1
West Ham wameizibua Hull City Bao 2-1 na kuchupa hadi Nafasi ya 11 katika Msimamo wa Ligi Kuu England.
West Ham walikuwa wa kwanza kupata Penati ya Mark Noble katika Dakika ya 26, Penati ambayo ilitolewa baada ya Kipa Allan McGregor kumwangusha Mohamed Diame na kupewa Kadi Nyekundu.
Hull City waliwasazisha katika Dakika 48 kwa Bao la Nikica Jelavic lakini ushindi ukawa kwa West Ham kwa Bao la James Chester aliejifunga mwenyewe katika Dakika ya 54. 
LIGI KUU ENGLAND
MSIMAMO:
NA  TIMU  P  W  D  L  F  A GD PTS
1 Chelsea 31 21 6 4 62 23 39 69
2 Liverpool 31 21 5 5 84 39 45 68
3 Man City 29 21 3 5 79 27 52 66
4 Arsenal 31 19 6 6 54 35 19 63
5 Everton 30 16 9 5 46 30 16 57
6 Tottenham 31 17 5 9 40 40 0 56
7 Man United 31 15 6 10 48 37 11 51
8 Newcastle 31 14 4 13 38 43 -5 46
9 Southampton 31 12 9 10 45 40 5 45
10 Stoke 31 9 10 12 36 45 -9 37
11 West Ham 31 9 7 15 34 41 -7 34
12 Aston Villa 30 9 7 14 33 42 -9 34
13 Hull 31 9 6 16 33 39 -6 33
14 Norwich 31 8 8 15 26 48 -22 32
15 Swansea 31 7 9 15 41 47 -6 30
16 West Brom 30 5 13 12 33 45 -12 28
17 Crystal Palace 30 8 4 18 19 39 -20 28
18 Sunderland 29 6 7 16 27 45 -19 25
19 Cardiff 31 6 7 18 26 58 -32 25
20 Fulham 31 7 3 21 30 70 -40 24
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumamosi Machi 29
1545 Man Utd v Aston Villa
1800 Crystal Palace v Chelsea
1800 Southampton v Newcastle
1800 Stoke v Hull
1800 Swansea v Norwich
1800 West Brom v Cardiff
2030 Arsenal v Man City
Jumapili Machi 30
1530 Fulham v Everton
1800 Liverpool v Tottenham
Jumatatu Machi 31
2200 Sunderland v West Ham

Monday, March 24, 2014

EL_CLASSICO-MACHI_23WAKALI wa Spain, Real Madrid na Barcelona, walishuka Jana Usiku katika dimba la uwanja Estadio Santiago Bernabeu naBarcelona kuibuka kidedea kwa Bao 4-3 huku Lionel Messi akipiga Hetitriki, Penati 3 zikifungwa na, kama kawaida, Kadi Nyekundu kwa Sergio Ramos.
MAGOLI:
Real Madrid 3
-Dakika ya 20 & 24  Karim Benzema
-Dakika ya 55 Ronaldo [Penati]
FC Barcelona 4
-Dakika ya 7  Andres Iniesta
-Dakika ya 42, 65 & 84 Lionel Messi [Penati 2]
Licha ya ushindi huo, Atletico Madrid ndio wako kileleni wkifuatiwa na Real Madrid na Barca wapo Nafasi ya 3, Pointi 1 nyuma ya Real na Atletico.
Huko Spain, Timu zikifungana Pointi, kinachohesabiwa ni Matokeo ya Mechi zao, Uso kwa Uso, ni si Magoli na kama hilo litafungana ndio Magoli huhesabiwa.
LA LIGA
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Atletico de Madrid
29
22
4
3
66
21
45
70
2
Real Madrid CF
29
22
4
3
80
30
50
70
3
FC Barcelona
29
22
3
4
85
25
60
69
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Barca ndio waliotangulia kufunga kwa Bao la Iniesta na Real kujibu kwa Bao mbili za Karim Benzema na kisha Messi akasawazisha na Gemu kuwa 2-2 hadi Haftaimu.
Ndipo Kipindi cha Pili zikaja Penati 3, nyingine za utata, wakati Ronaldo alipofunga Bao la 3 kwa Penati, Messi kusawazisha kwa Penati na kisha kufunga Bao la ushindi kwa Penati zikiwa zimebaki Dakika 6.
VIKOSI:
REAL MADRID [Mfumo: 4-3-3]:
Lopez,
Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo;
Xabi Alonso, Luka Modric, Di Maria
Gareth Bale, Karim Benzema, Cristiano Ronaldo,
Akiba: Casillas,  Varane, Fábio Coentrão, Nacho, Morata,  Isco,  Illarramendi
BARCELONA [Mfumo: 4-3-3]:
Valdes,
Jordi Alba, Pique,Mascherano, Alves
Xavi, Iniesta, Busquets,
Messi, Neymar, Fabregas,
Akiba: Pedro, Sánchez, Pinto Colorado, Bartra, Song, Adriano, Sergi
Refa:  Alberto Undiano Mallenco
WATAZAMAJI: 85,454
LA LIGA
Uso kwa Uso
26/10/13, 18:00 FC Barcelona 2-1 Real Madrid
02/03/13, 16:00 Real Madrid 2-1 FC Barcelona
07/10/12, 19:50 FC Barcelona 2-2 Real Madrid
21/04/12, 20:00 FC Barcelona 1-2 Real Madrid
10/12/11, 22:00 Real Madrid 1-3 FC Barcelona
16/04/11, 22:00 Real Madrid 1-1 FC Barcelona
29/11/10, 21:00 FC Barcelona 5-0 Real Madrid
10/04/10, 22:00 Real Madrid 0-2 FC Barcelona
29/11/09, 19:00 FC Barcelona 1-0 Real Madrid
02/05/09, 20:00 Real Madrid 2-6 FC Barcelona
13/12/08, 22:00 FC Barcelona 2-0 Real Madrid
07/05/08, 22:00 Real Madrid 4-1 FC Barcelona
23/12/07, 19:00 FC Barcelona 0-1 Real Madrid
10/03/07, 22:00 FC Barcelona 3-3 Real Madrid
22/10/06, 21:00 Real Madrid 2-0 FC Barcelona
01/04/06, 22:00 FC Barcelona 1-1 Real Madrid
19/11/05, 20:00 Real Madrid 0-3 FC Barcelona
10/04/05, 19:00 Real Madrid 4-2 FC Barcelona
20/11/04, 22:00 FC Barcelona 3-0 Real Madrid
25/04/04, 19:30 Real Madrid 1-2 FC Barcelona

Friday, March 21, 2014

MAN UNITED YAPANGWA NA BAYERN MUNICH ROBO FAINALI CHAMPIONS LEAGUE


Mechi za Robo Fainali kuchezwa Apirili 1 & 2, Marudiano Aprili 8 & 9
Droo ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI iimefanyika huko Nyon, Uswisi na Mabingwa Watetezi Bayern Munich watakutana na Mabingwa wa England, Manchester United, na Mechi ya Kwanza kuchezwa Old Trafford Aprili 1 au 2.
Chelsea watakuwa Ugenin kucheza na Paris Saint-Germain.
Barcelona wataanza kwao Nou Camp kwa kucheza na wenzao wa Spain Atletico Madrid.
Real Madrid wataanza Nyumbani Santiago Bernabeu kwa kucheza na Klabu ya Germany Borussia Dortmund.
Mechi za Marudiano zitachezwa Wiki moja baadae.
Barcelona v Atletico Madrid
Real Madrid v Borussia Dortmund
Paris St Germain v Chelsea
Manchester United v Bayern Munich
Mechi kuchezwa April 1/2 and April 8/9

VPL, LIGI KUU VODACOM YANGA KUIKABILI RHINO YA TABORA


YANGA, RHINO KUCHEZA TABORA VPL
Yanga inaumana na Rhino Rangers katika moja kati ya mechi mbili za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitakazochezwa wikiendi hii katika miji miwili tofauti.
Mechi hiyo itafanyika kesho (Machi 22 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, mjini Tabora ambapo kiingilio kitakuwa sh. 5,000 kwa jukwaa kuu na sh. 3,000 mzunguko.
Nayo JKT Ruvu itakuwa mwenyeji wa Mbeya City katika mechi itakayochezwa kesho Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Jumapili) kwa mechi nne ambapo Simba itacheza na Coastal Union katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Azam itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Azam Complex. Mechi hizo mbili zitakuwa ‘live’ kupitia Azam Tv.
Mechi nyingine za Jumapili ni Mgambo Shooting dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, wakati Ruvu Shooting na Ashanti United zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
20
12
8
0
27
44
2
Yanga SC
19
11
7
1
29
40
3
Mbeya City
21
10
9
2
10
39
4
Simba SC
21
9
9
3
17
36
5
Kagera Sugar
21
8
8
5
3
32
6
Ruvu Shooting
20
7
7
6
-4
28
7
Coastal Union
21
5
11
5
1
26
8
Mtibwa Sugar
21
6
8
7
-1
26
9
JKT Ruvu
21
8
1
12
-13
25
10
Prisons FC
20
3
10
7
-4
19
11
Mgambo JKT
20
4
6
10
-17
18
12
Ashanti United
21
4
6
11
-18
18
13
JKT Oljoro
21
2
9
10
-16
15
14
Rhino Rangers
21
2
7
12
-14
13
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano Machi 26
Mgambo JKT v Azam FC
Yanga v Tanzania Prisons
Jumamosi Machi 29
Ashanti United v JKT Oljoro
Jumapili Machi 30
Mbeya City v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar v Coastal Union
JKT Ruvu v Rhino Rangers
Azam FC v Simba
Mgambo JKT v Yanga
KIKOSI KAZI KUSHUGHULIKIA TIKETI ZA ELEKTRONIKI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na benki ya CRDB zimeunda kikosi kazi (task force) kwa ajili ya kushughulikia matumizi ya tiketi za elektroniki ambayo yalisimamishwa kutoka na changamoto mbalimbali zilizokuwa zimejitokeza.
TFF na CRDB zimefanya kikao cha pamoja jana (Machi 20 mwaka huu) kuhusu masuala ya tiketi za elektroniki na kukubaliana kuunda kikosi kazi hicho kwa ajili ya uboreshaji matumizi ya mfumo huo.
Kikosi kazi hicho kitakuwa na wajumbe kutoka TFF na CRDB. Kwa upande wa TFF wajumbe wake ni Mkurugenzi wa Sheria na Uanachama, Evodius Mtawala, Ofisa Habari na Mawasiliano, Boniface Wambura na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Silas Mwakibinga.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi ametoa shukrani za kipekee kwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dr. Charles Kimei ambaye alihudhuria binafsi kwenye kikao akiongoza timu yake.
Malinzi amesema ni imani ya TFF kuwa mfumo wa tiketi za elektroniki ndiyo mkombozi wa ulinzi wa mapato milangoni, na anaamini kwa pamoja TFF na CRDB zitafanikisha matumizi hayo ya tiketi za elektroniki.