Friday, March 28, 2014

BODI YA LIGI YASEMA SINGANO LAZIMA ALE KIBANO

Wakati Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likisubiri taarifa kutoka serikalini kuhusu thamani ya kioo cha mlango kilichovunjwa na winga wa Simba, Ramadhan Singano ‘Messi’, Bodi ya Ligi imesema kuwa lazima Messi akumbane na rungu jingine kutoka kwao.
Bodi hiyo imesema kuwa inataka kutoa adhabu hiyo ili iwe kama fundisho kwa wengine kwani kilikuwa ni kitendo cha kudhamiria.
Messi alivunja kioo hicho Jumapili iliyopita baada ya timu yake kuchezea kichapo cha bao 1-0 mbele ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa, ambapo hasira za kufungwa akazihamishia kwenye mlango wa vyumba vya kubadilishia nguo kwa kuupiga teke.
Ofisa Mtendaji wa Bodi la Ligi, Silas Mwakibinga alisema licha ya mchezaji huyo kulipa fidia za kioo hicho, bodi watakaa kuangalia ni adhabu gani atatakiwa kupewa kama onyo.
“Lilikuwa tukio ambalo kila mmoja aliliona, siyo kusema ilikuwa bahati mbaya, hivyo baada ya mambo mengine kumalizika, suala lake haliwezi kuachwa hivihivi, kuna adhabu nyingine itatolewa kama fundisho kwa wote,” alisema Mwakibinga.
Tayari mchezaji huyo ameomba radhi kwa kitendo chake kwa kile alichosema zilikuwa ni hasira za kukosa mabao ya wazi, hususan dakika ya mwisho alipobaki na mlinda mlango wa Coastal.

BPL:ARSENAL KUIKARIBISHA MAN CITY UWANJANI EMIRATES".

Kesho Jumamosi Ligi Kuu nchini uingereza inaingia tena kilingeni kwa michezo 7 kuanzia Mechi ya Saa Tisa na dakika 45 katika uwanja wa Old Trafford kati ya Manchester United na Aston Villa na kumalizika Usiku kwa Bigi Mechi Uwanjani Emirates kati ya Arsenal na Man City.
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumamosi Machi 29
15:45 Man United v Aston Villa
18:00 Crystal Palace v Chelsea
18:00 Southampton v Newcastle
18:00 Stoke v Hull
18:00 Swansea v Norwich
18:00 West Brom v Cardiff
20:30 Arsenal v Man Cit
Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, licha ya kukaririwa kukiri kwamba wao hawana nafasi ya kutwaa Ubingwa, ametamka kwamba bado lengo lao ni kuwa Mabingwa.
Amesema: “Hatuna kitu kingine zaidi ya kuwa Bingwa! Hiyo ndio azma yetu ya kwanza!”
Lakini Arsenal wanapambana na Man City ambayo iliwakung’uta Bao 6-3 Mwezi Desemba katika Mechi ya Ligi Uwanjani Etihad.
Wenger amesisitiza ni muhimu kwao kuonyesha nguvu Nyumbani kwao na hilo ndio litakalodhihirisha kama wana nafasi ya Ubingwa.
MSIMAMO:
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Chelsea 31 21 6 4 62 23 39 69
2 Liverpool 31 21 5 5 84 39 45 68
3 Man City 29 21 3 5 79 27 52 66
4 Arsenal 31 19 6 6 54 35 19 63
5 Everton 30 16 9 5 46 30 16 57
6 Tottenham 31 17 5 9 40 40 0 56
7 Man United 31 15 6 10 48 37 11 51
8 Newcastle 31 14 4 13 38 43 -5 46
9 Southampton 31 12 9 10 45 40 5 45
10 Stoke 31 9 10 12 36 45 -9 37
11 West Ham 31 9 7 15 34 41 -7 34
12 Aston Villa 30 9 7 14 33 42 -9 34
13 Hull 31 9 6 16 33 39 -6 33
14 Norwich 31 8 8 15 26 48 -22 32
15 Swansea 31 7 9 15 41 47 -6 30
16 West Brom 30 5 13 12 33 45 -12 28
17 Crystal Palace 30 8 4 18 19 39 -20 28
18 Sunderland 29 6 7 16 27 45 -19 25
19 Cardiff 31 6 7 18 26 58 -32 25
20 Fulham 31 7 3 21 30 70 -40 24
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumapili Machi 30
1530 Fulham v Everton
1800 Liverpool v Tottenham
Jumatatu Machi 31
2200 Sunderland v West Ham

Thursday, March 27, 2014

TFF YAANZA KUENDELEZA UWANJA WAKE MNYANJANI, TANGA

TFF YAANZA KUENDELEZA UWANJA WA TANGA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeanza mchakato wa kuendeleza uwanja wake uliopo eneo la Mnyanjani jijini Tanga.
TFF_LOGO12Shughuli inayoendelea kwa sasa ni kupima udongo (soil test) na kuandaa michoro kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha michezo (Sports Complex) ukiwemo uwanja wa mpira wa miguu na majukwaa yake.
TFF imetuma maombi rasmi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kuomba eneo la kujenga kituo cha michezo ikiwemo uwanja wa mipira wa miguu na majukwaa yake.
Pia Mkuu wa mkoa ameombwa kuingilia kati kuwaondoa wafanyabiashara waliovamia uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri (King George Memorial ground) mjini Moshi.
TFF YAANZA KUENDELEZA UWANJA WA TANGATFF inawakumbusha viongozi wa vyama vya mikoa ambao hawajaomba maeneo ya kujenga vituo vya michezo vikiwemo viwanja vya mpira wa miguu, waongeze jitihada za kufanya hivyo, TFF itawaunga mkono.
TFF inachukua fursa hii kuvipongeza vyama vya mpira wa miguu ambavyo ama tayari vimeshachukua hatua au viko mbioni kuchukua hatua kutafuta na kuendeleza maeneo kwa ajili ya matumizi ya mpira wa miguu.
TFF inaahidi kuunga mkono juhudi hizi na pale itakapohitajika kuongeza nguvu haitasita kufanya hivyo.
Wakati huo huo, TFF inalishukuru Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kwa kukubali kugharamia uwekaji nyasi za bandia kwenye Uwanja wa Kaitaba, na pia kusaidia uendelezaji wa uwanja wa TFF wa Tanga.
JAMAL MALINZI
RAIS
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

BPL-LIVERPOOL YAITUNGUA SUNDERLAND YAKWEA NAFASI YA PILI

Liverpool jana usiku imefanikiwa kuibuka na ushindi kwa Bao za Steven Gerrard na Daniel Stirridge zimewapa Liverpool ushindi wa Bao 2-1 walipocheza na Sunderland kwenye Mechi ya Ligi Kuu England na kuzidi kuwapa matumaini ya kuweza kutwaa Ubingwa Msimu huu.
Bao la Sunderland lilifungwa na Ki Su

WEST HAM 2 HULL CITY 1
West Ham wameizibua Hull City Bao 2-1 na kuchupa hadi Nafasi ya 11 katika Msimamo wa Ligi Kuu England.
West Ham walikuwa wa kwanza kupata Penati ya Mark Noble katika Dakika ya 26, Penati ambayo ilitolewa baada ya Kipa Allan McGregor kumwangusha Mohamed Diame na kupewa Kadi Nyekundu.
Hull City waliwasazisha katika Dakika 48 kwa Bao la Nikica Jelavic lakini ushindi ukawa kwa West Ham kwa Bao la James Chester aliejifunga mwenyewe katika Dakika ya 54. 
LIGI KUU ENGLAND
MSIMAMO:
NA  TIMU  P  W  D  L  F  A GD PTS
1 Chelsea 31 21 6 4 62 23 39 69
2 Liverpool 31 21 5 5 84 39 45 68
3 Man City 29 21 3 5 79 27 52 66
4 Arsenal 31 19 6 6 54 35 19 63
5 Everton 30 16 9 5 46 30 16 57
6 Tottenham 31 17 5 9 40 40 0 56
7 Man United 31 15 6 10 48 37 11 51
8 Newcastle 31 14 4 13 38 43 -5 46
9 Southampton 31 12 9 10 45 40 5 45
10 Stoke 31 9 10 12 36 45 -9 37
11 West Ham 31 9 7 15 34 41 -7 34
12 Aston Villa 30 9 7 14 33 42 -9 34
13 Hull 31 9 6 16 33 39 -6 33
14 Norwich 31 8 8 15 26 48 -22 32
15 Swansea 31 7 9 15 41 47 -6 30
16 West Brom 30 5 13 12 33 45 -12 28
17 Crystal Palace 30 8 4 18 19 39 -20 28
18 Sunderland 29 6 7 16 27 45 -19 25
19 Cardiff 31 6 7 18 26 58 -32 25
20 Fulham 31 7 3 21 30 70 -40 24
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumamosi Machi 29
1545 Man Utd v Aston Villa
1800 Crystal Palace v Chelsea
1800 Southampton v Newcastle
1800 Stoke v Hull
1800 Swansea v Norwich
1800 West Brom v Cardiff
2030 Arsenal v Man City
Jumapili Machi 30
1530 Fulham v Everton
1800 Liverpool v Tottenham
Jumatatu Machi 31
2200 Sunderland v West Ham