Friday, April 25, 2014

MIAKA 20 WA KENYA WATUA KUIVAA NGORONGORO HEROES

TIMU ya vijana ya Kenya inatarajiwa kuwasili nchini leo (Aprili 25 mwaka huu) saa 1 usiku tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Tanz

ania (Ngorongoro Heroes).
Mechi hiyo ya marudiano ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 itachezwa Jumapili (Aprili 27 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 2,000 na sh. 5,000.

Kenya na Ngorongoro Heroes zilitoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyochezwa Machakos wiki tatu zilizopita.
Mshindi baada ya mechi ya marudiano atacheza na Nigeria katika raundi itakayofuata.
Ngorongoro Heroes inaendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo chini ya Kocha John Simkoko. Mechi hiyo itachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi wakiongozwa na Pacifique Ndabihawenimana wakati Kamishna ni Tarig Atta Salih kutoka Sudan.

TAIFA STARS VS BURUNDI MAKOSHA WAAHINDI SOKA SAFI

MAKOCHA wa timu za Taifa za Tanzania (Taifa Stars) na Burundi (Intamba Mu Rugamba), Salum Mayanga na mwenzake Niyungeko Alain Olivier wameahidi burudani ya nguvu kwenye mechi yao itakayochezwa kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo ya kirafiki ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar itachezeshwa na refa Anthony Ogwayo kutoka Kenya na itaanza saa 10 kamili jioni.
Ogwayo atasaidiwa na Gilbert Cheruiyot na Oliver Odhiambo wote pia kutoka Kenya.

Mwamuzi wa mezani atakuwa Israel Mujuni wa Tanzania wakati Kamishna ni Charles Ndagala.
Mayanga amesema wanatumia mechi hiyo kama sehemu ya maandalizi ya mechi za mchujo za Kombe la mataifa ya Afrika, na ameahidi kuchezesha baadhi ya wachezaji waliopatikana kwenye mpango wa maboresho ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
Naye Niyungeko amesema amekuja na kikosi imara ambacho pia kitakuwa na washambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe na Didier Kavumbagu wa Yanga, lengo lao ni kuhakikisha wanapata ushindi kwa vile Taifa Stars imekuwa ikiwasumbua kila wanapokutana nayo.

Viingilio katika mechi hiyo ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000.

Wakati huo huo, Kocha Mkuu mpya wa Taifa Stars, Martinus Ignatius Maria maarufu kama Mart Nooij atatambulishwa kwa waandishi wa habri kesho Jumamosi (Aprili 26 mwaka huu) saa 8 kamili mchana kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa.



Thursday, April 24, 2014

KOCHA MPYA STARS KUTUA JUMAMOSI

MKENYA OGWAYO KUCHEZESHA STARS, BURUNDI
Mwamuzi Anthony Ogwayo mwenye beji ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kutoka Kenya ndiye atakayechezesha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Burundi (Intamba Mu Rugamba) itakayochezwa keshokutwa (Aprili 26 mwaka huu)  Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ogwayo katika mechi hiyo ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, atasaidiwa na Gilbert Cheruiyot na Oliver Odhiambo wote pia kutoka Kenya. Mwamuzi wa mezani atakuwa Israel Mujuni wa Tanzania.

Burundi inatarajia kuwasili nchini leo (Aprili 24 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya Kenya Airways na itafanya mazoezi kesho (Aprili 25 mwaka huu) saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Taifa.

Nayo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ipo kambini jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi hiyo ambayo itakuwa ya kwanza tangu kuanza kwa mpango wa maboresho wa timu hiyo.
Makocha wa timu zote mbili pamoja na manahodha wao kesho (Aprili 25 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia mechi hiyo.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000.
KOCHA MPYA STARS KUTUA JUMAMOSI
Kocha Mkuu mpya wa Taifa Stars, Martinus Ignatius Maria maarufu kama Mart Nooij anatarajiwa kuwasili nchini Jumamosi alfajiri (Aprili 26 mwaka huu) tayari kwa ajili ya kuanza kazi ya kuinoa timu hiyo.

Nooij (59) atawasili saa 7.20 usiku kwa ndege ya Ethiopia Airlines ambapo anatarajia kukutana na waandishi wa habari Jumamosi mchana, saa chache kabla ya kuanza mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Burundi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
                                          BONIFACE WAMBURA
                                     OFISA HABARI NA MAWASILIANO
                            SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Wednesday, April 23, 2014

MTIBWA IPO MBIONI KUTOLEA MACHO WANANDINGA WAPYA

Timu ya soka ya Mtibwa Sugar Mabingwa wa zamani wa Tanzania kwa mwaka 1999 na 2000wamekiri kukumbana na changamoto kubwa msimu wa 2013/2014 wa ligi kuu Tanzania bara uliomalizika aprili 19 mwaka huu .
 Afisha habari wa klabu hiyo, Tobias Kifaru Lugalambwike ameueleza mtandao huu kuwa kitu kikubwa walichojifunza ni maandalizi makubwa ya baaadhi ya timu zinazoshiriki ligi kuu toafuti na wao.
“Sisi ni wakongwe katika ligi hii, lakini tumeshindwa kuonesha cheche kutokana na kuwepo kwa timu zenye kiwango kizuri. Mbeya City fc wametikisa kweli, sio kwetu tu hata Simba na Yanga wamekumbana na upinzani na ndio maana wamekosa ubingwa ”.
“Kikubwa tumebaini changamoto zetu ikiwemo kukosa wachezaji muhimu kikosini. Tunataka kufanya usajili mzuri ili tuanze maandalizi ya mapema”.

BURUNDI KUTUA KESHO NCHINI KUIKABILI STARS

Timu ya Taifa ya Burundi (Intamba Mu Rugamba) inatarajiwa kuwasili nchini kesho (Aprili 24 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya Kenya Airways tayari kwa mechi dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumamosi (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Intamba Mu Rugamba it
Burundi-CECAFA-Teamakuwa na msafara wa watu 28 wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi na viongozi, na itafikia hoteli ya Accomondia. Mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 10 jioni
Nayo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ipo kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach ikijiandaa kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Kenya.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000. Mechi hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

MALINZI AWAPA PONGEZI SUKER, LEKJAA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewapongeza marais Davor Suker na Fouzi Lekjaa kwa kuchaguliwa tena hivi karibuni kuongoza mashirikisho ya mpira wa miguu katika nchi zao.
Suker amechaguliwa tena kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Croatia (CFF) wakati Lekjaa amechaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Morocco (FRFM).
Katika salamu zake za pongezi, Rais Malinzi amesema ushindi waliopata ni uthibitisho kuwa familia ya mpira wa miguu katika nchi zao ina imani kubwa kwao katika kuendeleza mchezo huo ndani na nje ya nchi hizo.
Rais Malinzi amesema Lekjaa na Suker wana uwezo wa kuendeleza kazi nzuri ambayo tayari imefanyika, lakini vilevile kuja na mawazo mapya ambayo yatakuwa changamoto kwa ustawi wa mchezo huo nchini Morocco na Croatia kwa ujumla.