
ania (Ngorongoro Heroes).
Mechi hiyo ya marudiano ya michuano
ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 itachezwa Jumapili (Aprili 27
mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Viingilio katika mechi hiyo
vitakuwa sh. 2,000 na sh. 5,000.
Kenya na Ngorongoro Heroes zilitoka
suluhu katika mechi ya kwanza iliyochezwa Machakos wiki tatu zilizopita.
Mshindi
baada ya mechi ya marudiano atacheza na Nigeria katika raundi itakayofuata.
Ngorongoro Heroes inaendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo chini ya Kocha John Simkoko. Mechi hiyo itachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi wakiongozwa na Pacifique Ndabihawenimana wakati Kamishna ni Tarig Atta Salih kutoka Sudan.
Ngorongoro Heroes inaendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo chini ya Kocha John Simkoko. Mechi hiyo itachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi wakiongozwa na Pacifique Ndabihawenimana wakati Kamishna ni Tarig Atta Salih kutoka Sudan.